Gesi ya
Chlorine ilitumika katika kuwashambulia watu Kaskazini mwa Syria mwaka
huu, hii ni kwa mujibu wa shirika la kimataifa ambalo linanuia kuweka
sheria zinazoharamisha silaha za kemikali.
Shirika hilo, (OPCW) linasema lina ushahidi kuonyesha kuwa gesi ya Chlorine ilitumika katika kuwashambulia wakazi .
Shambulizi
lilifanyika mapema mwaka huu, katika vijiji vilivyo karibu na maeneo
ambako waasi wamekuwa wakipigania na wanajeshi wa serikali.
Shirika la OPCW limekuwa likijihusisha na juhudi za kuharibu silaha za kemikali nchini Syria.
Mwaka
mmoja uliopita, Syria ilitangaza kuharibu silaha za kemikali zilizokuwa
zimewekwa nchini humo kuambatana na sheria za kimataifa.
Hata hivyo, Syria haikushurutishwa kutangaza kiwango cha silaha ilizonazo, ambazo zinaonekana kuwa za kemikali.
Ripoti
hii ya hivi karibuni inasma kuwa kemikali za sumu zilitumiwa
kuwashambulia watu vijijini hasa katika maeneo yaTalmanes, Al Tamanah na
Kafr Zeta Kaskazini ya Syria.
Kadhalika ripoti hiyo inasema kuwa inaamini kwamba kemikali ya Chlorine ndiyo iliyotumika katika kuwashambulia wanakijiji.
Inasema
wanajua kwamba ni gesi ya Chlorine iliyotumika kutokana na dalili
walizokuwa nazo wanakijiji , walivyokuwa baada ya matibabu pamoja na
maelezo kuhusu gesi hiyo.
No comments:
Post a Comment