viongozi wa dini |
Mkuu wa
jimbo la kusini Mashariki Ihemi katika kanisa la Kiinjili la kilutheri
Tanzania (KKKT) dayosisi ya Iringa mchungaji Aikam Chavalla akimshukuru
mbunge wa jimbo la Kalenga Godfrey Mgimwa kwa kuendelea kuchangia
maendeleo ya jimbo la kalenga (picha na Francis Godwin)(Victor Simon)
Na Francis Godwin Blog
VIONGOZI
wa dini na wazee katika jimbo la Kalenga mkoani Iringa wameeleza
kufurahishwa na utemndaji kazi wa mbunge wa jimbo la Kalenga Bw Godfrey
Mgimwa na kuwa wao kama viongozi wa dini kazi yao kubwa ni kuendelea
kumwombea ili azidi zaidi ili kuendelea kuwatumikia wananchi wa Kalenga.
Wakizungumza
kwa nyakati tofauti jana baada ya mbunge huyo kufanya ziara katika
makanisa mawili ya kata ya Ifunda likiwemo kanisa la Romanicathoric (RC)
parokia ya Ifunda na kanisa la Kiinjili la kilutheri Tanzania (KKKT)
usharika wa Ifunda kibaoni viongozi hao walisema wamepata kuwa na
wabunge zaidi ya wanne katika jimbo hilo ila utendaji wa Mbunge umekuwa
na matumaini makubwa kiasi cha wananchi kujivunia uwajibikaji wa mbunge
wao.
Mkuu wa
jimbo la kusini Mashariki Ihemi katika kanisa la Kiinjili la kilutheri
Tanzania (KKKT) dayosisi ya Iringa mchungaji Aikam Chavalla alisema kuwa
kwa zamani jimbo hilo ilikuwa ni vigumu kwa mbunge kuitwa kwa dharula
kanisani na kufika kushiriki na wapiga kura wake .
Pia
alisema wao kama viongozi wa dini wamekuwa wakifanya kazi kwa karibu na
viongozi mbali mbali wa serikali hasa ukizingatia kuwa wote ni viongozi
ila kila mmoja anamtegemea mwenzake katika kuongoza na kuwa wakati
viongozi wa serikali na wabunge wanawakilisha watu katika utawala wa
umma na wao viongozi wa dini wapo kwa ajili ya kuwaombea wote kufika
katika ufalme wa mbinguni.
Hivyo
alisema kuwa jimbo la Kalenga litaendelea kuwa na maendeleo iwapo
viongozi wote wataiga mfano wa mbunge Mgimwa katika kuwatumikia wananchi
badala ya wabunge wengine ambao walikuwepo kwa ajili yao pekee.
Kwa
upande wake paroko wa kanisa la RC Ifunda Alois Mdemu alisema kuwa
mchango wa kiongozi huyo katika maendeleo unafanana na ule wa marehemu
babake mbunge aliyefariki Dr Wiliam Mgimwa ambae pia alikuwa akijitoa
zaidi kwa ajili ya wananchi wake.
Paroko
Mdemu alisema kuwa mbali ya kuwa Godfrey Mgimwa ni mbunge kijana ila
kazi anayoifanya inaonyesha si kijana tena bali ni baba wa wananchi wote
wa Kalenga na hivyo iwapo ataendelea hivyo wana kalenga kamwe
hawatajisikia yatima kwa kuondokewa na mbunge wao Dr Mgimwa.
Mbali ya
viongozi hao wa dini pia wazee wa kata ya Ifunda wamesema kuwa kutokana
na utendaji wa mbunge huyo hadi sasa hawahitaji mbunge mwingine zaidi ya
Mgimwa katika jimbo hilo ila hawawazuii wanaofika kuchangia maendeleo
ya jimbo hilo kuunga mkono wa mbunge wao Mgimwa.
Akizungumza
kwa niaba ya wazee wenzake mwenyekiti wa kikundi cha Vicoba cha wazee
Ifunda BEatus Mduda alisema kuwa uanzishwaji wa kikundi hicho
umechangiwa kwa kiasi kikubwa na mbunge huyo na kuwa toka nchi ipate
uhuru jimbo la kalenga halijapata kuwa na mbunge ambae amewakumbuka
wazee kama Mgimwa na kuwa wao kama wazee hawaoni sababu ya kuwa na
mbunge zaidi yake tena .
"Tunatambua
umri wako bado kijana hivyo hata tukiendelea kukuchagua kwa vipindi
zaidi ya vinne bado nguvu ya kututumikia wananchi wa Kalenga unayo hivyo
sisi wazee tayari tumeanza kuwashawishi vijana wetu kuwapuuza wale wote
wanaojipitisha jimboni kutaka ubunge na tunaomba CCM kuwashughulikia
wote wanaofanya kampeni za ubunge"
Mbunge
Mgimwa alisema kuwa katika ziara yake hiyo ndani ya kata ya Ifunda na
kijiji kimoja hicho cha ifunda kibaoni amechangia kiasi cha Tsh milioni
4.5 kwa ajili ya kwaya ya Mtakatifu Secilia katika kanisa la RC kiasi
cha Tsh milioni 2 ,mchango kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya muziki
kanisa la KKKT Ifunda kiasi cha Tsh milioni 1 na mchango kwa ajili ya
uanzishwaji wa vicoba kwa kikundi hicho cha wazee kiasi cha Tsh milioni 1
na kuwa ataendelea kufanya hivyo kwa wananchi wake wa kata na vijiji
vyote iwapo watamshirikisha.
No comments:
Post a Comment