Siku tatu
kabla ya Bunge la Katiba kuanza kupigia kura Rasimu ya Katiba
inayopendekezwa,
watu wasiojulikana wameanza kusambaza vitisho vya
kuwatia hofu wajumbe
wa Bunge hilo.
Watu hao
wamesambaza vipeperushi katika maeneo mbalimbali ya mji wa
Dodoma
usiku
wa kuamkia jana, wakiwataka wajumbe kutoingia bungeni vinginevyo
yatakayowapata watajuta, huku wajumbe kutoka Zanzibar wakitishiwa kwa
ujumbe
wa simu kupitia mtandao wa WhatsApp.
Tayari,
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd ametoa kauli
kuhusu vitisho hivyo akisema Serikali itachukua kila hatua kuhakikisha
wajumbe
kutoka visiwani humo ambao wamekuwa wakipokea vitisho wanakuwa
salama.
Mbali na
kusambazwa kwa karatasi hizo, maandishi mekundu yamechorwa katika
kuta
za jengo la Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma yakisomeka, "No Katiba.
No
ufisadi."(T.K)
Vikaratasi
vilivyosambazwa vinasomeka: "Onyo. Dodoma si mahali pa
kufuga wezi wa
fedha za umma. Utakayeingia bungeni kuanzia kesho (leo),
yatakayokupata
utajuta."
Mkazi wa
Dodoma, Sospeter Samwel alimwambia mwandishi wetu jana
kuwa aliokota
baadhi ya vipeperushi hivyo jana saa moja asubuhi katika
eneo maarufu la
kuuzia magazeti linalotazamana na Jengo la CCM.
"Tulikuta
hayo makaratasi yametupwa tu ovyoovyo ila baadaye nikasikia
maeneo
mbalimbali mengine nayo yameonekana yametupwa. Sijui nani
hasa watakuwa
wameyasambaza," alisema.
Katibu wa
Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alipoulizwa jana kuhusu
na
maandishi hayo alijibu kwa kifupi "No comment" (sina cha kusema).
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime jana alitoa taarifa ya
maandishi
kwa wanahabari akisema jeshi hilo linawasaka watu waliosambaza
vipeperushi hivyo.
"Wananchi
na wageni wapenda amani waendelee na shughuli zao
kama kawaida kwani
polisi tumejiimarisha ipasavyo kukabiliana na
yeyote atakayekiuka sheria
na maelekezo yaliyotolewa.
Mkuu wa
Mkoa wa Dodoma, Dk Rehema Nchimbi alitoa onyo kwa
watu aliodai wanafanya
mzaha akisema vyombo vya usalama viko
macho saa 24. Aliwataka wajumbe
kutoa taarifa kwa vyombo vya
dola wanapoona viashiria vya kutokuwa na
usalama.
"Kama
ng'ombe mzima tumeshakula tumebakiza mkia tu, niwahakikishie
wajumbe wa
Bunge Maalumu la Katiba, usalama umekuwapo na
utaendelea kuwapo.
Wazanzibari kulindwa
Akizungumzia
vitisho hivyo hasa kwa wajumbe kutoka Zanzibar, Balozi Idd
alisema
Serikali itachukua kila hatua kuhakikisha wanakuwa salama.
Alisema
kuna ujumbe unazunguka katika mitandao ya jamii ukitoa vitisho
kwa
wajumbe wa Bunge hilo na watumishi wa sekretarieti ya Bunge hilo.
"Vyombo
vya dola vipo na vitafanya kazi yake. Vinajua vitisho vyote.
Niwahakikishie wajumbe mtakuwa salama na Serikali itachukua kila hatua
kuhakikisha hakuna kitakachotokea.
Hoja 17 za Zanzibar
Akizungumzia
kuhusiana hoja 17 ambazo ziliwasilishwa na Mwanasheria
Mkuu wa
Zanzibar, Othman Masoud Othman zenye masilahi ya visiwa
hivyo, Balozi
Idd alisema kati yake 13 zilikubalika na kubakia nne.
Hata hivyo, alisema baada ya kuangalia zaidi Rasimu ya Katiba
inayopendekezwa
waligundua kuwa zilibakia hoja tatu tu.
Alizitaja hoja hizo kuwa ni ibara 86 ambayo inasema Rais wa Jamhuri ya
Muungano atashinda kwa kupata kura zaidi ya asilimia 50.
Hata
hivyo, alisema waliona kwenye Katiba ya sasa jambo hilo liko
kimya
kidogo endapo itatokea mgombea hakupata kura upande wa Zanzibar.
"Tukaona
kuwa huyu ni Rais wa Muungano, hivi asilimia 50 yote apate
Bara
legitimacy (uhalali)
yake kama rais wa Muungano iko wapi?" alisema na
kuongeza kuwa vyema
katika Rasimu ikaingizwa
kuwa mgombea huyo pamoja na
kwamba anatakiwa ashinde kwa zaidi ya
asilimia 50, basi angalau
katiba
iweke
kiwango fulani cha kupata upande wa Zanzibar.
Alisema
baada ya kutafakari ikakubaliwa Zanzibar angalau mgombea
huyo apate
asilimia 10 au 15.
Hata hivyo, alisema majadiliano kuhusu suala hilo
bado yanaendelea
No comments:
Post a Comment