Wake wa viongozi wa jumuiya ya Uamsho ambao waume zao wamewekwa ndani kwa zaidi ya miezi tisa wametaka kuchukuliwa hatua za kisheria katika uendeshaji wa kesi hiyo badala ya utashi wa kisiasa.
Wakizunguma na waandishi wa habari kiongozi wa wake hao 16 Asha Idd amesema uwamuzi wao huo sio kuingilia kazi za mahakama, lakini wanawajibu wa kukumbusha utekelezaji wa sheria kwenye kesi hiyo.
Amesema kitendo hicho cha kuwekwa ndani waume zao licha ya kuathiri familia zao kisaikolojia, lakini pia kinarudisha nyuma taaluma ya dini ya kislamu kutokana na waislamu wengi walihudhuria katika darsa zao..
Aidha Asha ameziomba taasisi za haki za binadamu ndani na nje ya nchi na rais wa Zanzibar Dr. Ali Mohammed Shein kuangaliwa mwenendo wa kesi za waume zao ili kuona haki inatendeka
No comments:
Post a Comment