- Written byTupambane Blog
-
Share on facebook Share on gmail Share on twitter
Geilson Santana ‘Jaja’ akishangilia goli na wachezaji wenzake.
Kiingilio
cha chini kwenye mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Yanga na
Simba itakayochezwa Jumamosi (Oktoba 18 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar
es Salaam ni sh. 7,000.
Mshambuliaji wa Simba Emmanuel Okwi akishangilia.
Washabiki
watakaolipa kiingilio hicho ni wale watakaokaa viti vya rangi ya bluu
na kijani ambavyo jumla yake ni 36,693 katika uwanja huo wenye viti
57,558. Viingilio vingine ni sh. 10,000 kwa viti vya rangi ya chungwa,
sh. 20,000 kwa VIP B na C wakati VIP A itakuwa sh. 30,000.
Tiketi
zitakazotumika kwenye mechi hiyo ni za elektroniki, na zimeanza kuuzwa
jana (Oktoba 13 mwaka huu). Tiketi zinapatikana kwa mtandao wa M-PESA,
CRDB Simbanking na maduka ya CRDB Fahari Huduma ambayo yapo zaidi ya mia
moja sehemu mbalimbali jijini Dar es Salaam
No comments:
Post a Comment