- Written by Tupambane Blog
-
Share on facebook Share on gmail Share on twitter
Ndugu zangu,
Katika
Siku hii ya Mwalimu, nitarejea hapa moja ya mazungumzo muhimu ya
kihistoria niliyopata bahati ya kuyafanya; ilikuwa ni jioni ya Januari
24, 2012 pale nilipokutana na Mama Mosi Tambwe ( sasa marehemu) nyumbani
kwake Tabora Mjini.
Mosi
Tambwe aliingia TANU akiwa na miaka 18. Ni mmoja wa wanawake mahiri sana
kisiasa wa enzi hizo. Mosi Tambwe alinisimulia, kuwa alianzia kwenye
TANU Bantu Group, hiki kilikuwa ni kikundi cha vijana ndani ya TANU,
ambacho baadaye kikawa TANU Youth League.
Kwa
kirefu kabisa Mosi Tambwe aliniambia majukumu yao kama vijana kwa wakati
huo. Ni wakati nchi ikiwa chini ya mkoloni. Akanielezea pia majukumu
hayo yalivyobadilika baada ya uhuru. Enzi hizo vijana walikuwa
wakiandaliwa kupitia TANU Youth League ili waje kuwa makada wa chama,
hivyo basi, viongozi wa wananchi walinolewa vema. Walijengewa uwezo wa
kujenga hoja.
Ni enzi
hizo, baada ya kutoka Chipukizi, hatua iliyofuata ni Tanu Youth League.
Wengine wakaenda JKT na hata Jeshini. Azma kubwa ilikuwa kujenga
Uzalendo na Umoja wa Kitaifa.
Kwanini Julius Nyerere alitokwa na machozi mkutanoni pale Tabora? Nilimwuliza Mosi Tambwe.
- Unajua, siku ile Mwalimu alisimama akiongea, na mbele yake kulikuwa na Kituo Cha Polisi. Juu kwenye paa ya jengo hilo alisimama askari wa kikoloni aliyekuwa akiufuatilia mkutano huo akiwa na silaha mkononi. Jambo lile lilimtia huzuni sana Mwalimu, alijikuta akitoa machozi. Aliniambia Mama Mosi Tambwe ( Pichani)(T.K)
- Unajua, siku ile Mwalimu alisimama akiongea, na mbele yake kulikuwa na Kituo Cha Polisi. Juu kwenye paa ya jengo hilo alisimama askari wa kikoloni aliyekuwa akiufuatilia mkutano huo akiwa na silaha mkononi. Jambo lile lilimtia huzuni sana Mwalimu, alijikuta akitoa machozi. Aliniambia Mama Mosi Tambwe ( Pichani)(T.K)
Na unapomsikiliza Mama Mosi Tambwe unaiona tofauti kubwa ya vijana wa wakati huo na wa sasa.
Tumekosea wapi?
Jibu; ni pale, kwa shinikizo la mabadiliko ya dunia , na kwa shingo upande, chama tawala kiliporidhia kurejesha mfumo wa vyama vingi mwaka 1992. CCM ikasahau kuratibu mabadiliko makubwa ya kikatiba ambayo yalipaswa yaendane na mabadiliko hayo ya kimfumo.
Jibu; ni pale, kwa shinikizo la mabadiliko ya dunia , na kwa shingo upande, chama tawala kiliporidhia kurejesha mfumo wa vyama vingi mwaka 1992. CCM ikasahau kuratibu mabadiliko makubwa ya kikatiba ambayo yalipaswa yaendane na mabadiliko hayo ya kimfumo.
Kimsingi,
hali tuliyo nayo sasa ya kuchanganyikiwa, hata kwenye hili la vyama
kuunda vikosi vya ulinzi badala vya kiitikadi. Hii inatokana na makosa
makubwa, kama Taifa, tuliyoyafanya mwaka 1992.
Nimeandika mara kadhaa, kuwa historia ni mwalimu mzuri, lakini, wakati ni mwalimu mzuri pia. Tujifunze kutokana na mabadiliko ya wakati. Katika wakati tulio nao sasa, vyama vya siasa havipaswi kujiundia vikundi vya ulinzi vyenye kupata hata mafunzo ya kijeshi. Ni ujasiri, kama viongozi wa sasa watazipa mgongo fikra hizi za kizamani na kuendana na mabadiliko ya wakati.
Tufanye nini?
Nimeandika mara kadhaa, kuwa historia ni mwalimu mzuri, lakini, wakati ni mwalimu mzuri pia. Tujifunze kutokana na mabadiliko ya wakati. Katika wakati tulio nao sasa, vyama vya siasa havipaswi kujiundia vikundi vya ulinzi vyenye kupata hata mafunzo ya kijeshi. Ni ujasiri, kama viongozi wa sasa watazipa mgongo fikra hizi za kizamani na kuendana na mabadiliko ya wakati.
Tufanye nini?
Kama
ningeombwa ushauri hii leo, basi, ningevishauri vyama vya siasa, kuwa
kwa haraka sana, viachane na harakati za kuunda vikosi au vikundi vya
ulinzi. Jukumu hilo liachiwe vyombo vya usalama, hususan Jeshi la
Polisi, na hata makampuni ya ulinzi yenye kutambulika kisheria.
Na vile
vilivyopo vivunjwe. Maana, vikundi hivi vya ulinzi ambavyo kimsingi ni
vikundi vya wanamgambo wa vyama ni maafa tunayoyaandaa wenyewe. Kama
hatutanguliza busara na hekima, basi, itakuwa ni suala la wakati tu
kabla hatujajikuta kwenye dimbwi la maafa makubwa. Tumeshaziona ishara.
Kwa vyama
vya siasa, badala ya kutumia muda na rasilimali zao kufyeka mapori ya
kuwaweka vijana kwenye ' makambi ya ukakamavu', umefika wakati sasa wa
kubadilika, kuachana na fikra hizo za kijima zenye kuturudisha nyuma
miaka 50.Huu ni wakati wa kuwajengea vijana wa vyama ' ukakamavu wa akili'.
Zimepita, zama za ' Umkhoto we Sizwe'. Hizi ni zama za ' Umkhoto we Mitwe'- Ni mapambano ya kutumia vichwa kwa maana ya akili.
Naam, ukiona zinduna na ambali iko nyuma.
No comments:
Post a Comment