- Written by Tupambane Blog
-
Share on facebook Share on gmail Share on twitter
Dereva
Boda boda ambao ni wananchama wa Chama cha Wananchi CUF wakiongoza
msafara wa mapokezi ya Prof Ibrahim Lipumba mara tu alipo wasili
Wilayani Tunduru akitokea Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma.Lipumba
yupo Mikoa ya Kusini inayojumuisha Ruvuma,Lindi na Mtwara kwa ziara
ya siku 16 ikiwa na dhumuni la kuimarisha chama pamoja kuhamasisha
wananchi kujitokeza katika daftari la wapiga kura na vitambulisho
vya taifa
Huu ni umati wa watu waliojipanga barabarani kumpokea prof Ibrahim Lipumba
Wakazi wa Tunduru ambao ni wanachama wa Chama cha Wananchi CUF, wakiwa katika msafara wa Mwenyekiti wa chama hicho,Prof Ibrahim Lipumba.(T.K)
Wanachama wa Chama cha Wananchi CUF wakiwa katika msafara wa mapokezi ya Mwenyekiti wa chama hicho,Prof Ibrahim Lipumba
wenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF,Prof Ibrahim Lipumba mwenye shati jekundu na kofia nyekundu akiwapungia mkono wanachama wa chama cha CUF mara tu baada ya kufika katika ofisi za CUF Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma
Polisi wakiwa katika ulinzi wa Prof Ibrahim Lipumba
Naibu Mkurugenzi wa Oganaizesheni Uchaguzi na Bunge wa Chama Cha Wananchi CUF – Shaweji Mketo akiwahutubia wakazi
wa wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma,kutokufanya makosa wakati
wauchaguzi wa serikali za mitaa uliotangazwa kufanyika Disemba 14
mwaka huu wahakikishe wanakipigia Chama cha Wananchi CUF
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF,Prof Ibrahim Lipumba akiwahutubia maelfu ya wananchi waTunduru waliojitokeza kumsikiliza katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja baraza la Iddi Tunduru mjini.
No comments:
Post a Comment