- Written by Tupambane Blog
- Tuma Maoni
-
Share on facebook Share on gmail Share on twitter
Alan Henning kushoto mda mchache tu kabla ya kukatwa kichwa na mtu aliyesimama kando yake.
Kundi la
wanamgambo wa kiislamu la Islamic state limetoa ukanda wa video
unaoonyesha mateka Alan Henning raia wa Uingereza akikatwa kichwa.
Henning
mwenye umri wa miaka 47 ambaye ni dereva wa texi kutoka kaskazini mwa
Uingereza alitekwa nyara mwezi Disemba mwaka uliopita alipokuwa
akilifanyia kazi shirika moja la kutoa huduma za misaada kwa wakimbizi
nchini Syria.
Kundi la
Islamic State ambalo limechukua udhibiti kwenye maeneo ya mpaka kati ya
Syria na Iraq tayari lishawaua waandishi wa habari raia wa Marekani
James Foley na Steven Sotlof pamoja na mfanyikazi wa kutoa huduma za
misaada kutoka Scotland David Haines.
Mapema
babake John Cantlie raia wa Uingereza ambaye anashikiliwa mateka na
wanamgambo wa Islamic State aliomba kuachiliwa kwa mwanawe.
No comments:
Post a Comment