Halmashauri
inalenga kutoa huduma za ugani kwa wakulima na wafugaji. Aidha inalenga
kuthibiti magonjwa mbalimbali yanayoathiri mifugo na mazao yake kwa nia
ya kuendesha kilimo chenya tija.
Halmashauri imeendelea kutoa huduma
za ushauri kwa wafugaji na wakulima ambao hupatapatiwa mafunzo ya aina
mbalimbali. Aidha, Wakulima na wafugaji hufanya ziara za mafunzo pia
kuhudhuria maonyesho mbalimbali kama vile maonyesho ya viwanja vya
Nanenane Morogoro.
Magonjwa ya mifugo yanaendelea
kudhibitiwa kwa kuogesha na kutoa chanjo dhidi ya magonjwa mbali mbali
ambapo Ng'ombe hupata chanjo ya chambavu na Kimeta, na chanjo ya Homa ya
Mapafu.
Chanjo mbali mbali za Kuku kama vile chanjo ya Gumboro (IBD) na chanjo ya Mdondo hutolewa.
|
No comments:
Post a Comment