Askari 54 wa jeshi la polisi nchini Tanzania wamefukuzwa kazi katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Novemba mwaka huu kutokana na kujihusisha na vitendo vya rushwa.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi Mh. Pereira Ame Silima amesema kuwa kila mwaka serikali inapoteza wafanyakazi wengi kutokana na kujihususha na vitendo vya rushwa.
Mh. Silima ameongeza kuwa askari wengi wakishahitmu na kuingia kazini licha ya viapo wanavyokula lakini wanageuka kuwa wahalifu hivyo jeshi la Polisi nchini limewafukuza askari wote waliokutwa na Tuhuma za Rushwa.
No comments:
Post a Comment