- Written by Tupambane Blog
- Tuma Maoni
-
Share on facebook Share on gmail Share on twitter
Jenerali, Honore Traore, mkuu wa majeshi ya Burkina Faso akitangaza kuchukua madaraka ya nchi.
Mgawanyiko
umeripotiwa ndani ya jeshi la Burkina Faso kuhusu ni nani anayefaa
kuliongoza taifa hilo kufuatia kujiuzulu kwa rais Blaise Campaore baada
ya miaka 27 uongozini.
Kituo
kimoja cha radio kilitangaza taarifa kutoka kwa naibu mkuu wa kikosi cha
kumlinda rais kanali Isaac Zida iliyosema kuwa amechukua jukumu la
kuliongoza taifa hilo.
Mkuu wa majeshi ya Burkina Faso Jenerali Honore Traore, (katikati),akitangaza kuchukua madaraka kwa waandishi wa habari.
Mkuu wa
majeshi ya Burkina Faso Jenerali Honore Traore, (kati kati),akizungumza
kwenyemkutano na waandishi habari kutangaza kwamba anachukua madaraka ya
nchi akiwa katika makao makuu ya jeshi mjini Ouagadougou, mji mkuu wa
Burkina Faso, Oct. 31, 2014.
Mapema
mkuu wa majeshi Honore Traore alitangaza kuwa alikuwa amechukua
usukaniBlaise Compaore alijiuzulu baada ya kushuhudia maandamano yenye
ghasia baada ya jitihada zake za kutaka kuliongoza taifa hilo kwa awamu
nyengine kupitia bunge kugonga mwamba.
Aliyekuwa rais wa Burkina Faso Blaise Campaore.
Akizungumza
hapo jana kanali Zida amesema kuwa Jenerali Traore hawezi kuliongoza
taifa hilo.''Nimechukua jukumu la kuliongoza taifa hili na serikali ya
mpito ili kuliendeleza na kuhakikisha kuwa kuna mabadiliko ya
kidemokrasia kwa njia ya amani'' alisema kanali Zida katika hotuba yake
katika runinga.
Chanzo: BBC
No comments:
Post a Comment