- Written by Tupambane Blog
- Tuma Maoni
-
Share on facebook Share on gmail Share on twitter
Walemavu Mkoani Iringa wakifurahia baada ya kukabidhiwa baskeli zao ikiwa ni msaada kutoka Neema Crafts
Mkurugenzi
Mtendaji wa Neema Crafts Bwana Benjamin Ray akitoa ufafanuzi juu ya
msaada wa baskeli walioutoa kwa walemavu wa Mkoani Iringa.
Na Simon Victor
Walemavu
mbalimbali mkoani Iringa hapo jana walipewa msaada wa baskeli arobaini
kutoka Neema Crafts ambao wako chini ya dayosisi ya Ruaha.
Mkurugenzi
mtendaji wa Neema Crafts bwana Benjamin Ray akizungumza kwenye
makabidhiano hayo alisema kuwa, Neema crafts ilianzishwa mwaka 2003
chini ya dayosisi ya Ruaha.(T.K)
Ilianza
ikiwa na viziwi watatu na walikuwa wakijishungulisha na utengenezaji wa
karatasi. Mwaka 2009 walijenga jengo ambalo wanalitumia kwa mgahawa na
mwaka 2011 waliongeza jengo jingine ambalo wanitumia kama nyumba ya
kulala wageni ambayo inasimamiwa na walemavu na kuwa nyumba ya kwanza ya
kulala wageni kusimamiwa na walemavu wa kuongea(Mabubu).
Bwana Ray
alisema miradi yao yote inasimamiwa na walemavu wa aina mbali mbali.Pia
Ray isema msaada wa baskeli waliotoa kwa walemavu ni zawadi waliyopewa
kutoka nchini Marekani katika jimbo la Minnesota.
Nae
Mwenyekiti wa Walemavu(CHAWATA) mkoani Iringa Bwana Shaabani Shomari
aliwashukuru Neema Crafts kwa msaada waliotoa kwao.Lakini akatatoa
angalizo kwa walemavu wote waliopata baskeli hizo wazitumie kwa
madhumuni yaliokusudiwa.
Pia
Katibu wa CHAWATA Mkoa wa Iringa Ndugu, Haruna Mbata amewapongeza Neema
Crafts kwa kuwa bega kwa bega na wao na msaada waliotoa ni chachu kwa
maendeleo ya walemavu Mkoani Iringa
No comments:
Post a Comment