Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Sunday, November 9, 2014

MIFUGO




 
Katika Mkoa wa Dar es Salaam upo ufugaji wa mifugo ya aina mbalimbali kwa wanyama wakubwa na wadogo, kwa ajili ya chakula , biashara, wanyamakazi na wanyama rafiki (pets). Shughuli za ufugaji zinafanyika kwa idadi maalum kutegemeana na aina ya mifugo, kwa kufuata utaratibu uliowekwa. Aidha ufugaji huu unasaidia kwa kiwango kizuri kutoa ajira kwa wakazi wa Mkoa wa Dar es Salaam, ufugaji huu unatakiwa uwe endelevu na wenye kuzingatia kanuni za ufugaji bora.
 
 
 
Huduma za ugani:
 
Huduma za ugani hutolewa na wataalam wa mifugo wa Serikali wa Halmashauri za Manispaa za Mkoa wa Dar es Salaam, pamoja na sekta binafsi katika klinik na vituo vya mifugo.
 
 
Indigenous cattle keeping are not prominent in the region. These supply the draught animals and others are reared for slaughtering and milk. In some periods few cattle are brought in from other regions for fattening and then slaughtered or exported to Arabian countries and Comoro. The region slaughters an average of 800-1000 cattle daily
 
 
Huduma zinazotolewa na Wataalamu wa Mifugo wa Serikali:-
  1. Kutoa tiba na kinga dhidi ya magonjwa ya mifugo
  2. Kutoa elimu na ushauri kwa wafugaji kuhusu kanuni za ufugaji bora
  3. Uhamilishaji (A.I.) na kupima mimba
  4. Ukaguzi wa nyama na ngozi
  5. Kutoa vibali vya kusafirisha mifugo
  6. kutoa vibali kwa watu walioumwa na mbwa/wanyama kuweza kupata chanjo ya kuzuia ugonjwa wa kichaa cha mbwa katika hospitali za binadamu.
 
Huduma zinazotolewa na wataalam wa sekta binafsi:
 
1.  Kutoa tiba na kinga dhidi ya magonjwa ya mifugo
2.  Kutoa elimu na ushauri kwa wafugaji kuhusu kanuni za ufugaji bora
3. Uhamilishaji (A.I.) na kupima mimba
 

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG