Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Sunday, November 16, 2014

Raia wa Marekani akatwa shingo na IS.

Raia

Peter Kassig mda mchache kabla ya kukatwa shingo na wapiganaji wa IS
Kanda moja ya video iliowekwa mtandaoni inaonyesha mauaji ya mtu wa kutoa huduma za misaada raia wa Marekani Abdul Rahman Kassig ambaye alikuwa anajulikana kama Peter Kassig kabla ya kutekwa nyara na wanamgambo wa Islamic State nchini Syria mwaka uliopita

Video hiyo inamuonyesha mawanamume mmoja anayeonekana kuwa mwanachama wa Islamic State akiwa na kisu mkononi na maandishi yanayosema kuwa Peter Kassig ameuawa.

Kanda hiyo pia ina picha za watu kadha waliouawa ambao wanasemekana kuwa wanajeshi wa Syria waliokuwa wametekwa nyara.

Marekani imesema kuwa inafanya juhudi za kubaini chimbuko la kanda hiyo.

Bwana Kassig ambaye anajulikana kama Peter alitekwa nyara mwaka uliopita.

Mnamo mwezi Octoba kanda nyengine ya video ya kifo cha mfanyikazi mwengine wa misaada kutoka Uingereza Alan Henning iliisha huku Kassig akitishiwa.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG