Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Wednesday, November 5, 2014

RUFAA YA PONDA YATUPILIWA MBALI, KESI YAKE YAAHIRISHWA


  • Share on facebookShare on google_plusone_shareShare on twitterShare on linkedin
Ponda akiingizwa kwenye basi la wafungwa kwa ajili ya kwenda Segerea.
Magari ya Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) yakiwa yametanda eneo la mahakama.
Askari wakiongoza msafara.(P.T)
Wafuasi wa Ponda wakiimba nyimbo mbalimbali nje ya mahakama.
Dola ikifanya mawasiliano kuimarisha ulinzi.
Ukaguzi mkali kwa kutumia kifaa maalumu ukifanyika katika mlango wa kuingilia Mahakama Kuu.
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, jana imetupilia mbali rufaa ya Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda iliyopelekwa na wakili wake Juma Nassoro ya kupinga hatia ya adhabu aliyohukumiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akidai kuwa hapakuwa na ushahidi wa kutosha wa kumtia hatiani kwa mashtaka yaliyokuwa yakimkabili.
Kesi nyingine ya uchochezi inayomkabili kiongozi huyo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambayo inasikilizwa na Jaji Augustine Shangwa imeahirishwa hadi Novemba 20, mwaka huu.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG