Wahenga walisema palipo na Miti hapana
wajenzi,ni vigumu kujua mtunzi wa methali hiyo alikuwa na maana gani
lakini walimu wangi wa Kiswahili hufundisha kwamba maana ya hiyo Methali
ni kwamba palipo na mali hakuna watu wa kuweza kuitumia (utilize), na
ukiangalia katika Dunia ya sasa ni kitu ambacho kikowazi kwa sababu
ukiangalia mataifa mengi yaliyoendelea sio kwamba yote yana mali asili
za kutosha mfano Norway,Marekani na nchi nyingine nyingi za Magharibi
zilizoendela.
Tanzania ni kati ya nchi chache Duniani
zilizojaliwa na mali asili za kutosha na kila aina. Mfano Ardhi yenye
rutuba, Hali nzuri ya hewa,Mito na Maziwa yenye Samaki, Wanyama Pori na
Milima ya aina mbali mbali ambavyo hivyo vyote ni vivutio vya Watalii
ambavyo kama vingetumika vema Taifa lingejipatia pato la kutosha
kuendeleza shughuli za kiserikali pamoja na jamii kwa ujumla, lakini
kwetu sisi ni tofauti, tuna matatizo mengi hata zaidi ya Nchi ambazo
hawana kitu chochote, na tatizo kubwa linalolikabiri Taifa kwa sasa ni
ajira kwa vijana.
Kwa mtazamo wa haraka haraka tunaweza kugawa
sababu zinaazosababisha ukosefu wa ajira kwa vijana Tanzania katika
makundii mawili.Kundi la kwanza ni zile sababu zote zinazosababishwa na
serikali kutokana na sera zake butu juu ya swala hili.Na sababu nyingine
ni zile zinazozosababishwa moja kwa moja na jamii ya Watanzania
wenyewe.
Katika kundi la kwanza mfano mzuri ni mfumo wa
elimu. Elimu ya Tanzania ina mapungufu ya kutosha, hii ni kwa sababu
kijana anapomaliza elimu ya sekondari ambayo ni ya msingi kabisa, huwa
hana ujuzi wowote wa kazi Wa-spanish husema,aina hiyo ya elimu (la
educacion` en Tanzania es muy teorica), kwa sababu sio wote anaopata
nafasi ya kuendelea na elimu ya juu, hii inasababisha kundi kubwa la
vijana kurundikana mitaani,na kuleta athari zingine kama ubakaji,
uporaji, madawa ya kulevya.
Sababu nyingine ni rushwa,sio watu wote wenye
uwezo wa kununua kazi, wakati mwingine mazingira yanatatanisha
mno.Mathalani, utakuta kijana ana vigezo vyote vya kazi, ila kwa vile
hana uwezo wa kutoa kitu kidogo,na kwa bahati mbaya masikini huyu hamjui
mtu ( pale anapo omba ajira) basi hana zake tena, na kama tujuavyo
sote kuwa rushwa ni adui wa haki kwa hiyo anakuwa amepoteza haki yake ya
msingi na kuletea taifa matatizo makubwa kama vile kujihusisha na
vitendo viovu. Ujambazi kwa mfano.
Zaidi ya hapo kuna tatizo la kutowapatia msaada
(support) vijana hasa wanapo anziasha vikindu vidogo-vidogo kwa ajili ya
kujiajiri wenyewe. Oh, wataanza kufuatiliwa juu ya ushuru ambao sio
halari bali ulio kwa ajiri ya masilahi ya wachache tu--wakati kuna
mashirika na viwanda vikubwa ambavyo hawalipi ushuru na zaidi ya hapo
viwango wanavyo wawekea hao vijana ni zaidi ya uwezo wao. Itakumbukwa
kuwa, Baba wa taifa katika moja ya hotuba zake alisema kwamba serikali
yetu ya sasa haikusanyi mapato kama inavyotakiwa inakaa tu kukimbizana
na wafanyabiashara wadogo wadogo ambao hawana lolote. Alikuwa anaisema
serikali ya awamu ya pili kitu ambacho kipo hata leo hii.
Tatizo jingine liko kwa waajiri. Wao wanavutiwa
saaaana na wazee kwa sababu wana walipa kiasi ambacho kinawasababisha
wapate faida ya kutosha wakijua ya kwamba kuajiri vijana ni migogoro,
kwa sababu watadai haki za msingi.
Sio hayo tu pia vijana nao wana matatizo yao
yasiyoelezeka kwa urahisi. Mfano, vijana walio wengi wanachagua kazi
hata sizolingana na ujuzi walio nao. Unakuta kijan hana ujuzi wowote na
analaumu kwamba serikali haifai, bila ya kujali ujuzi wake. Katika moja
yaa hotuba zake, Mheshimiwa Mkapa aliwahi kusema: Watanzania wasingoje serikali ifanye kila kitu, wanalo jukumu la kujiletea maendeleo wenyewe..., na zaidi ya hapo, tukirudi nyuma serikali ni nani kama sio sisi wenyewe.
Jambo la kushangaza ni kwamba serikali imeshindwa
kuanzisha vyanzo vya kazi kwa vijana,Tanzania tuna ardhi kubwa ya
kutosha na yenye rutuba jambo la msingi ni kuanzisha Plantation and
Agro-base Industries.Kwani viwanda vingapi tunaweeza kuanzisha kwa mazao
tunayo zaliisha na kuuza kwa Nchi jirani kama Kenya? Au ni ajira ngapi
tunaweza kutengeneza kama tunaweza kuanzisha viwanda kama hivyo, lakini
serikali haioni hilo zaidi ya hapo ina-imports kila kitu na hii inaleta
ushindani na uuwaji wa hata vile viwanda ambavyo vilikuwepo na kuongeza
watu wasiokuwa na kazi. Pia unakuta serikali ina-export primary products
na hizi ni kutoa ajira kwa hizo nchi ambazo zina nunua mali ghafi
kutoka tanzania.
Zaidi ya hapo Tanzania hatuna sheria ya kazi na
kama ipo haifatwi.Utakuta mtu ana miaka 70 bado yuko kazini, na wakati
kuna kijana mwenye miaka 23 au 28 hana kazi na wana ujuzi sawa. Mfano
mzuri ni juu ya uteuzi wa Balaza la Mawaziri lililofanyika hivi
karibuni, kwangu binfsi sielewi juu ya uteuzi wa huyu Mheshimiwa
saaaaaaaaana Kingunge Gombare Mwiru, kwa sababu wako vijana wa kutosha
na wenye akili inayochemka na wenye uwezo mkuwa wa kufanya kazi ila sisi
kama watanzania utakuta jambo kama hili hatulioni, na zaidi ya hapo
utakuta vyombo vya habari vinasifia kwamba Rais amewakumbuka wakongwe,
je kwanini wasiulize juu ya Rais kuwakumbuka vijana?
Hiyo haitoshi kuna mambo mengine tukifikiria au
ukimuuliza raia wa Nchi yeyote yule hatapata jibu cha zaidi atabaki
kucheka. Hivi ni nini kitambulisho chetu sisi Watanzania? Kwa sababu
hatuna vitambullisho vya uraia, na kupata pasipoti Tanzania ni
Kitendawili, mimi kama Mtanzania ni haki yangu ya msingi kupata pasipoti
kama kitambulisho au Kipande kama waitavyo wenzetu wa Kenya.
Jiulize ni watu wangapi (wageni-foreigners)
wanaishi na kufanya kazi kinyume na sheria nchini Tanzania hasa katika
maeneo ya mipakani? Nenda Tabora na Kigoma utaona jinsi Wanyarwanda
walivyojazana, nenda Namanga Wakenya na Wasomali walivyojazana. Baya
zaidi ni kwamba; hao wote wana ajira na kama sio Serikalini basi katika
Mashirika binafsi, au wanatumia Mali Asili za Tanzania kujiajiri wenyewe
kitu kinachopelekea kupunguza nafasi za ajira kwa watanzania. Sio nia
ya maada hii kupinga wageni kufanya kazi nchini-la hasha!, ila kwanza
watanzania wapewe kipaumbele,na kama watanzania wakizikataa hizo kazi
basi wageni waruhusiwe kuzifanya.
Hatuwezi kumalliza hii maada bila kuangalia
mchango wa Taasisi za Fedha katika ajira, ajira sio lazima iwe ya
serikali au kutoka katika Kampuni binafsi, unaweeza kujiajiri, lakini
turudi katika nchi yetu, Kuna Mabenki lukuki yanatoa mikopo ila tatizo
ni viwango vya Riba, viko juu sana, na ukizingatia sera ya riba ni
kwamba ukiweka pesa benk riba inapungua kadri pesa inavyozidi kukua, na
katika utoaji , riba iaongeezeka kadri mkopo unavyo pungua, sasa jiulize
ni biashara gani ambayo ni productive kiasi kwamba hao vijana wanaweza
kupata hiyo riba na bado kubakia na kiasi fulani kwa ajiri ya kuendeleza
miradi yao.
Mwisho, ushauri wa bure kwa ndugu zangu
Watanzania, kwamba kwa sasa tuko katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, na
siyo hiyo tu pia SADC na huko tuko katika mapambano ya kiuchumi, kwa
hiyo inabidi tuwe Wazalendo kwa bidhaa zetu. Maana yake ni kwamba,
tununue bidhaa za kitanzania ili kuinua uchumi wa Tanzania, na kutoa
ajira kwa vijana wetu ni dhahili kwamba kama sisi wenyewe tutashindwa
kununua bidhaa zetu nani atakuwa radhi kuzinunua, Wazungu wanasema
Charty starts from Home. Kwa sasa inakadiriwa kwamba East Africa ina
idadi ya watu wapatao milioni 95, ikiwa Uganda ni Milioni 26, Kenya 34
na Tanzania ni 35, kwa hiyo kwa simple mathematics utaona kwamba
tunaidadi kubwa ya watu ukilinga nisha na nchi zingine , na ni dhahiri
kwamba soko letu ni kubwa, kwa hiyo tusije tukafanya makosa
yaliyofanyika karibu miaka 40 iliyopita na EAC, kwani kuna baadhi ya
nchi zina maendeleo zaidi yetu kutokana na matunda ya hiyo miaka
1967-1977..
Zaidi ya hapo tunaomba Serikali ijaribu kulinda
masoko yetu na Viwanda vyetu vya ndani ili kupunguza Competition kwani
ni dhahiri kwamba Tanzania tunazalisha mali bora zaidi ya nchi zengine
ila tatizo ni kwmba tumepumbazwa na baadhi ya wajanja wachache wanaopata
faida kutokana na uingizaji wa bidhaa hizo. Lakini ukweli unabaki pale
pale kwamba mambo yako Bongo, na zaidi ya hapo tuko na Malighafi za
kutosha, Hongera Bibie Meghji, kwa hatua uliyochukua wakati wa
usafirishaji wa magogo nchi za nje. Ni mategemeo yangu na ya Watanzania
wengine kwamba hao Mawaziri wanao husika na Wizara hizo wataanza na moto
mkali, na kujitahidi kuendeleza Tifa katika misingi aliyoiacha Mzee
Ben.
No comments:
Post a Comment