Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Sunday, November 9, 2014

USHINDI UPO VIJANA WAKI-TANZANIA NA AFRICA


HUMPHREY POLEPOLE KIONGOZI WA VIJANA
Vijana tujaribu kuwatumia watu waliofanikiwa katika jamii kama mifano hai ya kushinda wote tuna wajua akina Nelson mandela ,Nyerere,Shaka sali na wengine wengi si kuiga mambo ya kimagharibi kwenye runninga tu ambayo katika maisha halisi hayatusaidii lolote leo hii vijana wengi ni mabingwa wa kukimbilia mijini wakati wameacha utajiri vijijini mwao na kuthibitisha ni mkubwa wayaudi ,wajerumani na wengineo huingia nchini mwetu na kuwekeza vijijini.
Kama wageni wanauona utajiri huo je wewe unaye lia njaa wakati upo bize na vijibarua vya mjini ambavyo haviwezi kukukimu wewe je utawezaje hata kuwa na familia ,sasa ni wakati wakushughulikia ipasavyo fursa zilizopo katika maeneo yetu hasa vijijini hapa napo wadau wa maendeleo hasa serkali,mashirika binafsi,tuwekeze vijijini ,leo si ajabu kusikia nina shirika la kilimo na nipata misaada kusaidia wakulima wadogo elimu wakati hilo shirika lipo mjini tunashangaa hao walengwa wako wanalima nini lami au kilimo cha ndani ya nyumba.

Ukweli uliopo hakuna mjanja wa karne hii kama kijana anayeweza kutumia vema muda na mazingira yake vizuri kwani hatajuta kwaajiri ya muda nakujiua eti maisha magumu,wakati huu ni hatari sana kuwa na rafiki anaye kushauri kushinda vijiweni eti ni sehemu bora kama ni mahali safi kwa mawazo basi maamuzi ya mataifa yangefanyika huko ,watanzania vijana tubadilike na tuingie kwenye mapambano ya wakati uliopo.

Anayehitaji kushinda lazima apambane ni si kupambana tu bali kuangalia mbele hapa namaanisha kuwa na malengo ambayo yatakupa nguvu ili usibabaishwe na kelele za watu na wengine kufikia kukutenga kwa kuwa na msimamo wako imara kwani utakapo fanikiwa na na wao utawasaidia lakini ukiwasikiliza na mwishowe ukashindwa kuwasidia wata kulani milele.
MHE ;JOHN MNYIKA[ MBUNGE ]KIJANA
Obama alipogombea nafasi ya kuwa seneta kwa mara ya kwanza alishindwa ,tena namweusi mwenziwe hakukata tamaa ,akarudia tena akapita na hatima hakuishia hapo tu akfika nafasi ya juu zaidi na kushika dola kuu duniani na kila mwafrika na asiye mweusi kumwona kuwa moja ya mshujaa wa kujivunia.

Basi ni muda wa vijana kujiona kuwa ni sehemu ya dunia na jamii intuhitaji tena kwa kiwango kikubwa sana kuliko vile tunavyojiona ili tuweze kukumboa nchi zetu hasa za dunia ya tatu sasa sisi tukijiremba wakati ndugu zetu wanakufa kwa njaa,kukosa matibabu,vita, na utapiamlo ni aibu kubwa kwani wazee wetu walipigana wakatulea leo wao watakuffa kwa aibu ni dhambi kubwa kwa muumba wetu.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG