Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Monday, December 15, 2014

MARTHA MWAIPAJA APANIA KUBURUDISHA

SAM_3999
“TAMASHA linafanyika siku maalum ambayo Yesu Kristo amezaliwa, nitatoa huduma kwa njia ya uimbaji naomba wakazi wa mikoa yote mitatu wafike kwa wingi wale ambao hawanifahamu pia watanifahamu siku hiyo na wataguswa na kupata ujumbe uliotukuka,” anasema mwimbaji Martha Mwaipaja.
Mwimbaji huyo anasema kuwa amejipanga vilivyo ikiwa pamoja na kufanya maandalizi ya hali ya juu huku akisistiza kuwa atafanya makubwa katika tamasha la Krismasi ambalo litakuwa la pili kufanyika.
Mwaipaja anasema kuwa anawaomba mashabiki wafike kwa wingi kwa sababu amepewa nafasi hiyo ya kulihubiri neno la Mungu kupitia uimbaji hivyo yupo kwa ajili yao ni vema wakajitokeza kwa wingi kupata upako.
“Naimba kwa ajili ya kumtumikia Mungu, natoa huduma kwa njia ya uimbaji hivyo watanzania wajitokeze siku hiyo muhimu ya kuzaliwa kwa Yesu naamini watafurahi kwa jinsi ninavyofanya maandalizi ya tamasha hili kubwa ambalo limepangwa kufanyika siku yenye Baraka za Mungu,” 
Mwimbaji huyo anayevuma na nyimbo zake nyingi ambazo anatarajia kuziimba katika tamasha hilo la aina yake aliziita atakazoimba kuwa ni pamoja na Tusikate ‘Tamaa’ ambako alisema kuwa anaupenda wimbo huo kwa sababu wengi unawatia moyo.
Anasema kuwa  mbali ya wimbo huo ambao  upo kwenye albamu yake ya kwanza pia anatarajia kuimba wimbo wa ‘Ombi langu’ambao unapatikana katika albamu yake ya pili huku akifafanua kuwa maana ya wimbo huo kuwa mungu ametengeneza njia katikati ya aliowakumbuka nay eye yumo.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG