Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Monday, December 1, 2014

Wasichana shupavu washinda wanaume

Msichana wa India
Video inayoonesha wasichana wawili wanafunzi wakipigana na vijana kwenye basi katika jimbo la Haryana kaskazini mwa India, imekuwa habari kubwa huko.
Wasichana hao wawili ambao ni ndugu, wanasema walisumbuliwa na vijana na walipolalamika walishambuliwa.
Katika mitandao ya jamii wasichana hao wanasifiwa na wamepewa jina la "shupavu wenye moyo" kwa kupigana kwa hamasa.
Wengine wanauliza kwanini abiria wengine hawakuingilia kati.
Wasichana kusumbuliwa hadharani limekuwa swala kubwa nchini India baada ya msichana kubakwa na hatimaye kufa kwenye basi mjini Delhi karibu miaka miwili iliyopita.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG