Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Friday, February 6, 2015

MASTAA WENYE SKENDO ‘LIVE’

Na Mwandishi Wetu
Zimebaki siku saba kumalizika kwa mwaka 2010, tukielekea kufunga wiki ya 51, orodha ya mastaa wa Bongo waliotia fora kwa skendo wanaanikwa.
The Udaku Master, Ijumaa linaanika staa mmoja baada ya mwingine na jinsi walivyovuma na skandali zao;

ELIZABETH MICHAEL ‘Lulu’
Ni staa mwenye umri mdogo ambaye alitikisa zaidi mwaka 2010. Aliandikwa kwa matukio yake ya kulewa kupita kiasi kwenye kumbi za starehe na kuvaa nusu uchi.

Lulu ambaye umri wake una utata, ikidaiwa yupo chini ya miaka 18, pia alihusishwa na matukio ya kimapenzi, kubwa zaidi likiwa lile la kutoka kimapenzi na mwanamuziki wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba.

Kama hiyo haitoshi, aliripotiwa mwaka huu kugombana na ‘sidanganyiki’ mwenzake, wakidaiwa kurushiana makonde kisa kikiwa ni penzi la ‘janki flani’ hivi.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG