Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Tuesday, March 3, 2015

Majeshi ya Iraq mbioni kuikomboa Tikrit

   

Tikrit ilikuwa mji wa pili baada ya Mosul uliotekwa na Islamic State
Serikali ya Iraq inasema kuwa wanajeshi wake wameanza kampeini ya kuwafurusha wapiganaji wa Islamic State kutoka mji wa Tikrit .
Mji huo mkuu wa jimbo la kaskazini la Salahuddin ulidhibitiwa na wanamgambo wa Islamic state Juni mwaka uliopita.
Serikai inasema kuwa wanajeshi 30,000 wakiwemo wapiganaji 200 wakujitolea wa kisuni pamoja na wakurdi wanaelekea mji wa Tikrit wakisadiwa na ndege za kivita .
Mwandishi wa BBC mjini Baghadad anasema kuwa ikiwa mji wa Tikrit utatekwa na serikali itawezesha wanamgambo wa Islamic State kusukumwa kwenda maeneo ya mbali ya kaskazini hadi mji wa Mosul ambao ndio mji mkubwa
zaidi ulio mikononi mwa wanamgambo hao.
Mji wa Tikrit uko kilomita 150kmKaskazini mwa mji wa mkuu wa Baghdad.
Tikrit ilikuwa mji wa pili baada ya Mosul uliotekwa na Islamic State
Runinga ya kitaifa ya Al-Iraqiya imetangaza ripoti iliyodai kuwa wapiganaji hao wa IS walikuwa wamebumburushwa kutoka viunga vya mji wa Salahuddin nje ya Tikrit lakini habari hizo hazijathibitishwa.
Waziri mkuu Haider al-Abadi alifanya mazungumzo na koo za waSalahuddin kabla ya kutangazwa kwa operesheni hii kubwa zaidi kuwahi kufanyika.
Hata hivyo hii si mara ya kwanza kwa jaribio kama hili kutokea mwaka uliopita operesheni ya kujaribu kuwang'oa IS ilitumbukia nyo'ngo huku mamia ya wapiganaji waliokuwa wakiunga serikali mkono wakiangamia mikononi mwa wapiganaji wa Islamic State.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG