Kilabu ya
Manchester United haiwezi kushinda taji la ligi kwa kuwa haina
mshambuliaji mwenye uwezo wa kufunga mabao 20 kwa msimu.
Meneja
Luois Van Gaal amesema kuwa mshambuliaji mwenye mabao mengi katika klabu
hiyo ni Van Persie mwenye mabao 10 pekee ikilinganishwa na Diego Costa
na Sergio Aguerro ambao wamefunga mabao 17 kila mmoja wao.
''Ni kweli'',alisema Van Gaal.
''Robin van Persie hawezi kukataa,Falcao naye hawezi kupinga na Rooney hachezi katika safu ya mashambulizi.
MKufunzi
huyo wa Old Trafford amekuwa akikosolewa kwa kumchezesha Wayne Rooney
katika kiungo cha kati,huku Radamel Falcao akipewa fursa chache kwa
madai kwamba hayuko shwari.
Van Gaal alisema:''Kwa sasa hatuna mshambuliaji ambaye anaweza kufunga mabao 20''.CHANZO:BBC
No comments:
Post a Comment