Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Sunday, March 1, 2015

Van Gaal:Man U haina mshambuliaji mzuri


  • Share on facebook Share on google_plusone_share Share on twitter Share on linkedin

Kilabu ya Manchester United haiwezi kushinda taji la ligi kwa kuwa haina mshambuliaji mwenye uwezo wa kufunga mabao 20 kwa msimu.
Meneja Luois Van Gaal amesema kuwa mshambuliaji mwenye mabao mengi katika klabu hiyo ni Van Persie mwenye mabao 10 pekee ikilinganishwa na Diego Costa na Sergio Aguerro ambao wamefunga mabao 17 kila mmoja wao.
''Ni kweli'',alisema Van Gaal.
''Robin van Persie hawezi kukataa,Falcao naye hawezi kupinga na Rooney hachezi katika safu ya mashambulizi.
MKufunzi huyo wa Old Trafford amekuwa akikosolewa kwa kumchezesha Wayne Rooney katika kiungo cha kati,huku Radamel Falcao akipewa fursa chache kwa madai kwamba hayuko shwari.
Van Gaal alisema:''Kwa sasa hatuna mshambuliaji ambaye anaweza kufunga mabao 20''.CHANZO:BBC

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG