Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Friday, May 15, 2015

ANDRE SCHURRLE NAYE KUPEWA MEDALI YA LIGI KUU ENGLAND


   Andre Schurrle anaweza kuwa ameondoka katika ligi kuu ya Uingereza na kwenda kucheza katika ligi ya nyumbani kwao Ujerumani tangu mwezi January mwezi huu – lakini jambo hilo halijaweza kumfanya akose nafasi ya kujikusanyia medali ya ubingwa wa Premier League.

Winga huyo wa kijerumani, ambaye alihamia Wolfsburg kutoka Chelsea wakati wa dirisha la majira ya baridi, aliichezea Chelsea mechi 14 msimu kabla ya kuhama – hivyo kupata uhalali wa kujipatia medali ya ubingwa wa EPL.
Sheria za EPL zinaeleza ili mchezaji awe na hadhi ya kupata medali ni lazima awe ameitumikia klabu yake zaidi ya mechi 5.
Schurrle hakuwa na ufahamu wa sheria hii, lakini wiki iliyopita kocha wa Chelsea Jose Mourinho alimpigia simu mchezaji huyo na kumpongeza kwa kujishindia medali ya ubingwa wa EPL baada ya Chelsea kutawazwa kuwa mabingwa wapya wa ligi hiyo.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG