Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Wednesday, May 20, 2015

West Brom waifunga Chelsea 3-0

Saido Berahino akishangilia goli
West Brom imewachabanga mabingwa ligi kuu ya England Chelsea jumla ya mabao 3-0 hali ambayo kwa sasa inaifanya klabu hiyo kukaa eneo salama zaidi dhidi ya kushuka daraja.
Katika mechi hiyo iliyochezwa, dimba la The Hawthons, Saido Berahino alikata utepe wa magoli kwa kufunga goli la kwanza mnamo dakika ya 9,na pia dakika ya 47 Berahino tena akaweka kimiani goli la pili kwa njia ya penati ,baada ya kuangushwa na John Terry eneo la adhabu na hivyo hadi mwisho wa mchezo West Brom 3 Chelsea mabingwa nunge. Kwa matokeo hayo West Brom sasa wamefanikiwa kukaa eneo salama kuepuka kushuka daraja,huku Chelsea wakiwa bado mabingwa. Kesho Arsenal watakwaana na Sunderland.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG