Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Sunday, January 4, 2015

habari tofautitofauti

MUME AMLIPUA KWA PETROL MKE WAKE BAADA YA KUKATAA KUPASHA MOTO CHAKULA

Matuko ya kupiga na kunyanyaswa wanawake bado yameendelea kuchukua nafasi katika nchi malimbali za Afrika.
Tumekuwa tukiona ripoti mbalimbali za matukio mabaya ya unyanyasaji, kutoka Kenya mwanaume mmoja amefunguliwa mashtaka baada ya jaribio la kutaka kumuua mke wake kwa madai alishindwa kumpatia chakula cha moto.
Mwanaume huyo Peter Muthii alimmwagia mkewe petrol akiwa amelala, akawasha moto na kumfungia ndani ambapo muda mfupi baadaye majirani walikuja kumwokoa na kumkimbiza hospitali.
Kisa cha tukio hilo kimetajwa kuwa ni baada ya mwanaume huyo kurudi nyumbani usiku na kumtaka mkewe kumpashia chakula lakini mkewe alimwambia apashe mwenyewe kitendo kilichomkwaza, akaamua kumlipua kwa kutumia petrol iliyokua chini ya kitanda chao.

MAGAZETI YA UDAKU LEO

2015-01-03_07.05.36_5c214.jpg

MAGAZETI YA MICHEZO NA BURUDANI

20_17d0c.jpg

MAGAZETI LEO JUMAMOSI TAREHE O3.O1.2O15

1_36d5b.jpg


VIJANA WATATU WALIOTAKA KWENDA IKULU WAISHIA RUMANDE DAR!

VIJANA watatu wanaoaminika kuwa ni wafuasi wa chama kikuu cha upinzani CHADEMA, wamekamatwa na polisi eneo la Magomeni Mapipa jijini Dar es Salaam leo Ijumaa Januari 2, 2014, baada ya jaribio lao la kufanya matembezi kutoka mkoa wa Geita wakielekea Ikulu ya Dar es Salaam kumuona Rais Jakaya Kikwete kufikisha malalamiko yao.
Kwa mujibu wa taarifa ya Mkuu wa Wilaya Kinondoni jijini Dar es Salaam, Jordan Rugimbana, vijana hao watatu, Juma Maganga, Khalifa Selemani na Athanas Michael, walielekezwa na maafisa usalama kumuona yeye DC baada ya kuwasili kwenye eneo lake la utawala wakitokea Geita, ili awape baraka za kwenda Ikulu. Lakini walipofika ofisini hapo, DC huyo alitaka kujua nini hasa kilichowafanya watembee safari ndefu kama hiyo?
DC Rugimbana alisema, walimweleza kuwa Mosi, Wanataka Kumnuona Rais ili wamueleze kuchukizwa kwao na vitendo vya viongozi kula rushwa na hakuna hatua dhabiti zinazochukuliwa dhidi yao, kukithiri kw amatumizi mabaya ya rasilimali za taifa, kukithiri kwa vitendo vya unyanyasaji dhidi ya raia, na kudai kurejeshwa kwa serikali ya Tanganyika.

WASTARA ASOMA DUA KUMUENZI SAJUKI

YANGA VETERANI YATWAA KOMBE LA PSPF BAADA YA KUINYUKA SIMBA VETERANI

Nahodha wa timu ya maveterani wa Yanga, Salvatory Edward, akipokea kombe kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Adam Mayingu, baada ya kuinyuka Simba Veterani kwa penati 5-4 kufuatia sare ya mabao 1-1 katika pambano la bonanza lililodhaminiwa na mfuko huo na kupigwa kwenye uwanja wa Bandari Tandika, wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam jioni Alhamisi Januari 1, 2015. Kufuatia ushindi huo Yanga veterani pia walijinyakulia kitita cha shilingi milioni 1, wakati watani wao wa jadi Simba, shilingi laki 5

RAIS KIKWETE AMTEUA DK. MIGHANDA MANYAHI KUWA MWENYEKITI MPYA WA BODI YA TANESCO

Simba Yasalim Amri kwa Mara ya Pili kwa Mtibwa Sugar. Yachapwa Bao 1--0 Kombe la Mapinduzi

Wachezaji wa timu ya Simba wakipasha moto misuli kabla ya kukaguliwa na Mgini Rasmin Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, wakati wa ufunguzi wa michuano hiyo ilioaza leo Uwanja wa Amaan Zanzibar.

MBUNGE WA MOROGORO MJINI MH ABOOD ATOA MILION 11 KUTATUA KERO YA MAJI MKUNDI MOROGORO

 Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mh Aziz Abood Akizindua Tawi la CCM la Wajasiriamali Bodaboda na Mama lishe lililopo Mgulu wa Ndege Kata Ya Mkundi Manispaa ya Morogoro.Mara Baada ya Kuzindua Tawi Hilo Mh Abood Aliongea na Wanachama wa Tawi Hilo Kisha Kuwaelekeza Kujiunga Kwenye Vikundi vya Wajasiriamali Yeye Atakuwa Tayari kuwawezesha Mitaji ya Kufanya Shuguli za Kujiletea Maendeleo.
 Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mh Aziz Abood Akiwa Meza Kuu Sambamba na Katibu wa CCM Kata Ya Mkundi tayari Kusikiliza Kero zinazowakabili wakati wa Kata Hiyo Ambapo walimwambia Wanakabiliwa na Kero Kubwa ya Umeme,Maji na Barabara.Aidha Mh Abood Akitoa Majibu Kuhusu Kero Hizo Alesema Kuhusu Umeme Serikali Imeiweka Kata Hiyo Kwenye Bajeti ya Serikali ya Mwaka huu .Kuhusu Maji Mh Abood alitoa Shilingi Milioni 11 Kwajili ya Kununua Vifaa vya Kuwezesha Kufikisha Maji katika eneo la Mgulu wa Ndege Kata ya Mkundi.Pia Alitoa Shilingi Milion 2 kwajili ya Mafuta Ili Greda la Manispaa ya Morogoro Kuweza Kuchonga Barabarfa Zote za Kata Hiyo.
 Mwenyekiti wa Mtaa wa Mgulu wa Ndege Kata ya Mkundi Jimbo la Morogoro Mjini Akisoma Risala yake Kwa Mbunge wa Jimbo Hilo Mh Aziz Abood. 
Mmoja wa Wakazi   wa Kata ya Mkundi waliojitokeza Kwa Wingi Kwenye Ziara ya Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Akieleza Kwa msisitizo Kero Kubwa Inayowakabili wakazi wa Kata Hiyo                   









  Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mh Aziz Abood  Akiandika Baadhi ya Keo ambazo wananchi wa Kata ya Mkundi walimweleza wakati wa Ziara yake ya kutembelea Kata za Jimbo la Morogoro Mjini.
 Wakazi wa Kata ya Mkundi wakimsikiliza kwa Makini Mbunge wao
Wakazi wa Kata ya Mkundi wakimshangilia Mh Abood mara Baada ya Kutatua kero Kubw ya kata hiyo tatizo la Maji. 
  Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mh Aziz Abood  Akijibu Baadhi ya Kero zinazowakabili wakazi wa Kata ya Mkundi.

NYALANDU AANZA KAMPENI ZA RAIS 2015 KANISANI, AMHUSISHA JK NA MAJINI

Jana kwenye ibada ya mkesha wa kuupokea mwaka mpya uliooneshwa live star TV, Waziri Nyalandu alijitokeza wazi na kuongea kikampeni akiomba waumini wa dini ya Efata kumchagua kuwa Rais.
Isitoshe, Nyalandu aliongelea utawala wa Rais Kikwete kuwa ni utawala unaolindwa na majini saba, ingawa hakufafanua alimaanisha nini, lakini alishangiliwa sana na waumini wa Efata.

MAGAZETI YA LEO IJUMAA TAREHE O2.O1.2O15

BAADA YA MISS TANZANIA KUFUNGIWA MIAKA MIWILI LUNDENGA AFUNGUKA


Siku kadhaa baada ya Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), kuifungia Kampuni ya Lino International kuendesha mashindano ya Miss Tanzania kwa miaka miwili, Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Hashim Lundenga amesema hatua hiyo

MKESHA WA MWAKA MPYA: KILA KONA UCHAGUZI MKUU

Makamu wa Rais Dk Mohamed Gharib Bilali akiwaongoza wakazi wa Dar es Salaam kusherehekea Mwaka mpya katika Uwanja waTaifa, Dar es Salaam. Kulia ni Mkuu wa Mkoa, Saidi Mecky Sadiki na kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya mkesha, Godfrey Mallase.Ujumbe mahususi wa jinsi ya kushiriki na kuvuka salama katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba ulitawala salamu za kuukaribisha mwaka 2015 zilizotolewa juzi na viongozi wa dini na Serikali katika maeneo mbalimbali nchini.Wakati viongozi wa dini wakijikita katika kuhamasisha haki kutendekea katika uchaguzi na kuepuka vitendo vinavyoweza kusababisha uvunjifu wa amani na Makamu wa Rais, Dk Mohamed Ghalib Bilal aliwataka wananchi kuwatosa wagombea wote watakaotumia rushwa kuwashawishi wawachague.Salamu hizo zilianza kutolewa juzi wakati wa mkesha na Serikali ilitahadharishwa kuzingatia haki, usawa na demokrasia katika kusimamia uchaguzi huo ili kuepuka machafuko hasa katika kipindi cha uchaguzi huo.

EWURA: MAFUTA KUSHUKA MWANZONI MWA MWEZI FEBRUARI..PIPA LILIKUWA LINAUZWA DOLA 110 SASA LINAUZWA DOLA 60

OBAMA NA FAMILIA YAKE WAMESHEREHEKEA HIVI KUUPOKEA MWAKA MPYA


Sherehe kubwa za mwaka kwa mwaka 2014 ni kama zimeisha juzi baada ya kuupokea mwaka mpya 2015, kila mmoja kasherekea kwa aina yake, Rais wa Marekani Barack Obama pamoja na familia yake nao walipata nafasi ya kutoka nje ya Ikulu ya White House na kwenda kuenjoy kama watu wengine.
Vacation ya Obama na familia yake imeendelea katika visiwa vya Hawaii, alikutana na watu mtaani akawapa salamu za mwaka mpya; “Happy New Year, everybody!“, akasalimiana nao halafu wakaendelea kula zao ice cream.
Picha zake na familia yake wakijienjoy hizi hapa.

DK WILLBROD SLAA NA MKEWE WAOMBEWA NA GWAJIMA KUSHINDA URAIS 2015

Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima (kushoto), wachungaji wa kanisa hilo na viongozi wengine wa ngazi ya juu, wakimwombea Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbrod Slaa (katikati) na mkewe Josephine Mushumbuzi ili aweze kufanikiwa katika harakati zake za Uchaguzi Mkuu utakaofanyika baadaye mwaka huu, wakati wa ibada ya kuukaribisha Mwaka Mpya, iliyofanyika kwenye viwanja vya kanisa hilo Kawe, Dar es Salaam, usiku wa kuamkia jana.

DIAMOND PLATNUM NA ZARI NDANI NDIO HABARI YA MJINI TAZAMA HAPA WAKIWA RWANDA KWENYE VIBE PARTY

Staa Diamond Platnumz ambaye jana alikuwa akipiga show kali pale nchin Rwanda akiwa na mpenzi wake Zari the Boss Lady na kwa mujibu wa mashabiki wa Uganda wanasema wanaona kama Zari Hassan ndie mwanamke wa maisha ya Diamond Platinumz kutokana na yeyekujali sana kazi za mpenzi wake ambapo wamekuwa wakisafiri kila mara licha ya kwamba Zari anabishara zake lakin yuko Radhi kuziacha na kumpa Company mpenzi wake, Zari ambaye amempita Diamond kwa miaka kama 15 lakin siku zote umri ni namba tu kibwa ni Penzi acha Ubuyu uendeelee

MSIMAMO WA LIGI KUU YA UINGEREZA BAADA YA MECHI ZA JANA


LIGI KEE ENGLAND : CHELSEA WACHAPWA NA TOTTENHAM 5

Diego Costa gave Premier League leaders Chelsea a lead after striking into an unguarded net at Tottenham on New Year's Day
Oscar slid a clever ball back to the Spain international to tap home in front of a stunned White Hart Lane 

SHABIKI MWENYE HASIRA ATAKA KUVAA WENGER, WALINZI WAMUWAHI

SHABIKI MMOJA ALISHINDWA KUJIZUIA AKATAKA KUMVAA KOCHA ARSENE WENGER BAADA YA ARSENAL KUPOKEA KIPIGO CHA MABAO 2-0 KUTOKA KWA SOUTHAMPTON WALIOKUWA NYUMBANI. HATA HIVYO WALINZI WA UWANJA WA ST MARY WALIMUWAHI NA KUMUONDOA SHABIKI HUYO.

BUSH KUIONGOZA MAREKANI KAMA RAIS KWA MARA NYINGINE!

Gavana wa zamani wa Jimbo la Florida nchini Marekani Jeb Bush ametangaza kujiuzulu mnafasi mbalimbali ambazo anashika kwenye makampuni kadhaa pamoja na nyadhifa anazoshika kwenye bodi za taasisi mbalimbali zisizo za kibiashara ikiwa ni ishara ya dhamira ya gavana huyo wa zamani ya kuingia moja kwa moja kwenye mbio za kuwania urais katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka 2016 .
Kwa mujibu wa msaidizi wa karibu wa mwanasiasa huyo , Jeb ambaye ni mdogo wa rais wa zamani wa Marekani George Walker Bush ataangalia uhusiano alio nao kwneye biashara tofauti katika kipindi cha mwaka mwaka huu akiwa na lengo la kujiondoa kwenye biashara na kuingia kikamilifu kwneye siasa akiwania nafasi ya kukiwakilisha chama cha Republican kwenye uchaguzi wa mwakani 
Jeb Bush alitangaza mwishoni mwa mwaka 2014 kuwa anafuatilia kwa karibu mchakato wa urais japo hajaweka wazi azma yake ya kuingia kwenye mbio hizo .

REAL MADRID NJIA NYEUPE KUMSAJILI NTO HUYU!

Kiungo mshambuliaji wa Borrusia Dortmund Marco Reus huenda akashindwa kutimiza ndoto yake ya kujiunga na Fc Barcelona baada ya klabu hiyo kushindwa kwenye rufaa yake ya kupinga adhabu ya kuzuiwa kufanya usajili katika madirisha mawili yajayo ya usajili . 
Dortmund italazimika kumuuza nyota huyo ambaye ana kipengele kinachomruhusu kuondoka endapo timu yoyote itakuja na dau la euro milioni 25 , kipengele ambacho kitaweza kutumika baada ya kumalizReus ambaye inafahamika wazi kuwa ataondoka Dortmund msimu ujao aliwahi kuiahidi Barcelona kuwa atajiunga na klabu hiyo baada ya kumalizika kwa msimu huu lakini ahadi hiyo huenda ikashindwa kutimia kwani Barcelona wako chini ya adhabu ya Fifa ya kutosajili mchezaji yoyote kwa vipindi viwili vya usajili baada ya kukutwa na hatia ya kukiuka kanuni za usajili kwa wachezaji wenye umri chini ya miaka 18. 

Thursday, January 1, 2015

ARSENAL WAICHAPWA NA SOUTHAMPTON 2

Per Mertesacker stretches to try and hook Sadio Mane's shot off the line but can only touch the ball into his own net
Mane celebrates putting Southampton into the lead but the Senegalese striker was forced off injured just moments later
Southamtpon, who went into the game in fourth place, but only ahead of their opponents on goal difference, celebrate Mane's opener


No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG