Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Tuesday, January 6, 2015

SINGANO AIVUSHA SIMBA ROBO FAINALI KOMBE LA MAPINDUZI


SAM_4333

Kikosi cha Simba sc kilichoanza 
WEKUNDU wa Msimbazi wamefanikiwa kufuzu hatua ya robo fainali ya kombe la Mapinduzi kufuatia kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya vinara wa ligi ya Zanzibar, JKU katika mechi iliyomalizika usiku huu uwanja wa Amaan Zanzibar.Bao pekee la Simba limefungwa na Ramadhani Singano ‘Messi’ katika dakika ya 11 kwa shuti kali  akipokea pasi murua ya Said Ndemla.
SAM_4332
Kikosi cha JKU kilichoanza 
Kwa matokeo hayo, Simba wameibuka vinara wa kundi C kwa kujikusanyia pointi 6 kibindoni, huku nafasi ya pili ikishikwa na Mtibwa Sugar wenye pointi tanoSimba walianza mchezo kwa kasi, lakini JKU walionekana kuchakarika kuwadhibiti wakali hao wa Msimbazi.Kikosi cha Mnyama kinachonolewa na Mserbia Goran Kopunovic kimeonekana kucheza mpira wa kasi na pasi za uhakika kuanzia sehemu ya ulinzi na safu ya ulinzi.Baada ya mechi hiyo, kocha Kopunovic amesema timu yake inaimarika kidogo kidogo na ilicheza tofauti kwa vipindi vyote.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG