Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA
Showing posts with label WANYAMA. Show all posts
Showing posts with label WANYAMA. Show all posts

Tuesday, November 17, 2015

WANYAMA PORI

Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Adelhelm Meru akikagua mabegi matano yenye Kobe 201 yaliyokamatwa usiku wa kuamkia leo na askari wanyamapori kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama katika uwanja wa Kimataifa wa J.K. Nyerere jijini Dar es Salaam.  

Watuhumiwa hao wa usafirishaji wa wanyamapori wametajwa kuwa ni David Mungi mkazi wa Muheza Mkoani Tanga na Mohammed Suleiman (43) mkazi wa Zanzibar ambao katika tukio hilo walishafanikiwa kupita kwenye mitambo ya ukaguzi lakini mbwa maalum (sniffer dogs) wakasaidia kugundua uhalifu huo. Kwa pamoja watuhumiwa hao walikamatwa na tiketi za kusafiria kuelekea nchini Malaysia. 
Kobe wapatao 201 waliokamatwa na askari wanyamapori kwa ushirikiano na vyombo vya ulinzi na usalama kwa kutumia mbwa maalum (sniffer dogs).   
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Maliasili na Utalii Bi. Dorina Makaya kulia na Mmoja wa Askari wanyamapori wakiangalia kobe 103 waliotelekezwa eneo la Tabata hivi karibuni baada wahalifu waliohusika kuhofia kukamatwa na vyombo vya dola. 

Saturday, December 6, 2014

Wataka Sokwe apewe haki za kibinadamu

Sokwe Tommy anaaminika kuwa na umri wa miaka 40
Sokwe hawana haki sawa na binadamu na wala sio lazima wanyama hao kuachiwa huru na wale wanaowafuga. Hii ni kwa mujibu wa uamuzi wa mahakama nchini Marekani.
Uamuzi huu ulitolewa katika kesi kumhusu Sokwe kwa jina Tommy ambaye wanahakatari wa kutetea wanyama walitaka aachiliwe huru na mmiliki wake na pia atunzwe kama binadamu.
Jaji katika mahakama ya rufaa mjini New York aliyeisikiliza kesi hio, amesema Sokwe wanaokuwa wamefugwa hawawezi kutunzwa sawa na binadamu kwani hawawezi kuwajibishwa kama anavyoweza binadamu.
Shirika moja la kutetea haki za wanyama lilikuwa limedai kuwa Sokwe walio na usawa fulani na binadamu wanapaswa kuwa na haki sawa na na binadamu ikiwemo kupewa uhuru.
Shirika hilo limesema litakata rufaa katika kesi hiyo.
Katika uamuzi wake , jaji aliandika: '' Sokwe hawawezi kuwa na haki sawa na binadamu kwani hawawezi kuwajibishwa wala kupewa majukumu.''
Mahakama hio iliongeza kuwa hakuna sheria inayoshurutisha kwamba wanyama hao wapewe haki sawa na binadamu.
Mnamo mwezi Okotoba, shirika hilo la kutetea haki za wanyama, lilikuwa limetetea kwamba, Sokwe wanapaswa kutambuliwa kama binadamu katika sheria, na kisha kupewa haki sawa na uhuru kama binadamu.
Shirika hilo limesema litakata rufaa dhidi ya hukumu hio katika mahakama ya juu zaidi nchini humo

Thursday, November 6, 2014

HOTELI YA WANYAMA YAFUNGULIWA SINGAPORE

    • Share on facebookShare on google_plusone_shareShare on twitterShare on linkedin
    Hoteli moja ya kifahari ya wanyama wa kufugwa nyumbani imefunguliwa nchini Singapore.
    Hoteli hiyo inatoa huduma kama vile vidimbwi vya kuoga vya wanyama hao,vyumba vyenye hewa safi na vyakula vya kuvutia, na hivyobasi kuimarisha viwango vya kuwabembeleza wanyama hao katika taifa hilo lenye utajiri mkubwa.
    Hoteli hiyo yenye urefu wa futi 4,317 kwa jina Wagington Hotel imejengwa katika nyumba za zamani za wakolini wa Uingereza zilizobadilishwa katika makaazi ya wanadiplomasia.
    Vyumba vya kulalia katika hoteli hiyo vinagharimu dola 271 kwa mbwa watatu wanaotumia kwa pamoja chumba cha kifalme,kilicho na maeneo ya kifahari ya kuweka balbu,runinga,na vitanda vilivyotengezwa na ngozi.
    Hoteli hiyo iliojengwa hususan kwa mbwa pia huwakaribisha paka.
    ''iwapo tunajitakia mema katika maisha yetu, kwa nini marafiki zetu walio waaminifu nao tusiwafanyie mambo mazuri'' aliuliza mmiliki wa hoteli hiyo Estelle Taylor.
    ''Kama watu tunaowapenda wanyama,tuna hisi kwamba ni vyema kuwa na eneo ambalo wanyama wanaweza kuwekwa ili nao wajisikie nyumbani'' aliongezea.
    Wanaomiliki wanyama hao pia wanaweza kupata eneo la kufanya mafunzo,kunyoa, kukata kucha,kubadilisha rangi za wanyama hao pamoja na masaji.
    Hoteli hiyo pia hutoa huduma ya gari la kifahari aina ya Limousine kwa wanyama hao kutoka makaazi yao hadi hoteli hiyo na kutoka hoteli hiyo hadi makaazi yao.
    Nchini Singapore kuna zaidi ya maduka 250 ya wanyama, mengi yakiwa katika maduka makubwa ya jumla.
    Mfanyibiashara mmoja hutoa huduma za kitalii kila wikendi ambapo wamiliki wa wanyama hao na wanyama wenyewe hutembezwa katika mabot

    Saturday, October 18, 2014

    Twiga Wa Mikumi Huyu..

    • Written by Tupambane  Blog
    • Share on facebook Share on gmail Share on twitter 
    Asubuhi hii

    Sunday, October 12, 2014

    SIMBa wa Mikumi huyu....!

    • Written by Tupambane Blog
    • Share on facebook Share on gmail Share on twitter

    Simba huyu wa mikumi ni mpole sana, lakini upole wake haurefushi maisha yake,kwani si zaidi ya miaka 30 ataaga Dunia. Ni kikomo cha uhai wa mnyama Simba Picha na Hudugu Ng'amilo (T.K)

    Friday, August 22, 2014

    TUTUNZE WANYAMA WETU

    Bustani ya wanyama

    Matiger kwenye bustani ya wanyama
    Kitengo cha Panda kwenye bustani ya wanyama ya Chiang Mai (Uthai)
    Wageni wanalisha na kushika panyabuku waliozoea binadamu kwenye bustani ya wanyama ya Parc Animalier des Pyrenées, Ufaransa
    Twiga za Kiafrika huko Melbourne, Australia
    Bustani ya wanyama ni mahali ambapo wanyama hasa wanyamapori wa aina mbalimbali wanatunzwa ili watu wapate kuwatazama.
    Siku hizi bustani ya wanyama zimekuwa pia mahali pa kutunza spishi au aina za wanyama walioko hatarini kutokomea.
    Miji mingi mikubwa duniani ina bustani zaa wanyama. Katika baadi ya bustani hizi watu hulipa kiingilio wakitaka kuingia. Lakini hata hivyo bustani hizi hazipokei mapato ya kutosha hivyo hazina budi kupokea pia misaada kutoka serikali.
    Umuhimu wa bustani za wanyama ni katika
    • kuwapatia watu nafasi ya kuona kwa macho yao wanyama wa nchi zilizo mbali
    • kuwaelimisha watu juu ya wanyama wa dunia pia kuhusu mazingira yao
    • kuwa kituo cha utafiti wa kisayansi kuhusu wanyama
    • kuhifadhi na kufuga aina za wanyama hatarini kutokomea hasa wasio na mazingira asilia tena
    TUPAMBANE BLOG