Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA
Showing posts with label mlipuko wa magonjwa. Show all posts
Showing posts with label mlipuko wa magonjwa. Show all posts

Thursday, July 28, 2016

WAGONJWA 45,000 WA SARATANI HUGUNDULIKA TANZANIA KILA MWAKA

UG1
Mhe Ummy Mwalimu  akiwa na waziri wa afya (Uganda) Mhe .Sara Opendi na Mhe Omar Sey Waziri wa Afya wa  Gambia.
UG2
Waziri wa afya Ummy Mwalimu akifuatilia mkutano huo
UG3
Picha ya pamoja ya wake wa marais na mawaziri wa afya wa afrika,waliohudhuria mkutano wa 10 wa kupambana na saratani ya shingo ya Kizazi,matiti na tezi dume (picha/habari na wizara ya afya)
Na.Mwandishi wetu,Addis Ababa
Ugonjwa wa saratani nchini Tanzania  ni chanzo cha magonjwa na vifo,hivyo inakadiriwa Takribani wagonjwa wapya wa saratani 45,000 hugundulika kila mwaka.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu katika Mkutano wa 10 wa kupambana na ugonjwa wa saratani ya shingo ya kizazi, matiti na tezi dume barani Afrika unaofanyika nchini hapa.
Waziri Ummy amesema kati ya wagonjwa hao asilimia 38  ni wa saratani ya shingo ya kizazi kwa wanawake, asilimia 14  saratani ya ngozi, asilimia 10  saratani ya matiti na saratani ya tezi ni asilimia 4
Hatahivyo,takribani watu 35,000 hufariki kila mwaka kutokana na magonjwa ya Saratani.
Licha ya changamoto mbalimbali zinazokwamisha jitihada za kukabiliana na magonjwa hayo ikiwemo  uhaba wa Miundombinu ya kutolea huduma za afya, vifaa tiba, Uhaba wa Watumishi wa Afya, rasilimali fedha na gharama kubwa za dawa za matibabu ya saratani,Waziri Ummy amesema Serikali ya Tanzania  imepitisha Sera za Kitaifa na Miongozo mbalimbali ya Kupambana na Saratani, kutoe Elimu kwa jamii na watoa huduma za afya nchini kuhusu Saratani.
Aidha, kuanzishwa kwa huduma za upimaji wa saratani katika Hospitali na vituo vya afya zaidi ya 300 nchini na huduma za Tiba kupitia Hospitali ya Saratani ya Ocean Road.
“Serikali itapanua wigo wa matibabu ya saratani katika Hospitali ya Bugando Mwanza na KCMC, Kilimanjaro. Mipango ya baadae ni huduma hizo pia kutolewa ktk Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Mbeya.”hii itapunguza wagonjwa kufuata huduma kwenye hospitali ya saratani ya Ocean Road
Mkutano wa 10 wa Saratani ya shingo ya kizazi, matiti na tezi dume barani Afrika unafanyika kwa kuasisiwa kwa juhudi za wake za Marais wa bara la Afrika.
Mkutano huu unahudhuriwa na Wake wa Marais wa Afrika, Mawaziri wa Afya wa Afrika, Wanataaluma na Wadau wa Maendeleo. Lengo kuu ni kufanya mapitio ya hatua zilizochukuliwa na nchi za Afrika, changamoto zilizopo na kuweka mikakati ya pamoja na ya nchi katika kukabiliana na saratani.
Wakati wa kukabidhiwa uenyekiti wa Umoja wa Wake wa Marais wa Afrika wa Kupambana na saratani ya Shingo ya Kizazi, Matiti na Tezi Dume kutoka kwa Mwenyekiti anaemaliza muda wake, mke wa Rais wa Kenya mama Magreth Kenyatta, Mke wa Waziri Mkuu wa Ethiopia mama Roman Tesfaye Abneh ameleeza masikitiko yake kwa jinsi ambavyo ugonjwa wa saratani unavyoua kuliko hata ugonjwa wa UKIMWI na kifua kikuu. Hivyo ameziomba nchi za Afrika kuongeza uwekezaji katika eneo hili hasa kwa kuhakikisha dawa zinakuwepo za kutosha, kuboresha utoaji wa huduma za afya ikiwemo upimàji na tiba, kuhakikisha nchi zinatoa mafunzo ya Kutosha kwa watumishi  wa afya katika fani hii

Sunday, December 28, 2014

UGONJWA WA TB HATARI WAINGIA NCHINI


  • Share on facebook
    Share on google_plusone_shareShare on twitterShare on linkedin
Dar es Salaam. Wakati Taifa likikabiliwa na changamoto kubwa ya uhaba wa dawa hospitalini, aina mpya na hatari zaidi ya ugonjwa wa kifua kikuu sugu imegundulika na kuathiri mtu mmoja nchini.
Mgonjwa huyo alibainika kuwa na kifua kikuu sugu kisicho na tiba, aina ya 'Xtreme Drug Resistant' au XDR-TB ambayo hapo awali haikuwa ikiwaathiri Watanzania.
Huyu ni mgonjwa wa pili kubainika kuwa na aina hii hatari ya TB baada ya kesi ya kwanza kuripotiwa mwaka 2011.
Shirika la Afya Duniani (WHO) linaeleza kuwa XDR-TB ni nadra sana ambapo ni nchi 77 tu duniani ikiwamo Tanzania zimeripoti tatizo moja moja, mwishoni mwa mwaka 2011.
Taarifa zilizokusanywa na WHO kutoka katika mataifa mbalimbali duniani zinahakiki kuwa kuna asilimia tisa tu ya kesi za XDR-TB.
MDR-TB ni kifua kikuu sugu ambacho kimeshindikana kutibika kwa dawa za mstari wa pili.
Mratibu wa Ugonjwa wa Kifua Kikuu Mkoa wa Kinondoni, Dk Hassan Lupinda alithibitisha kupokewa kwa mgonjwa huyo na kusema kuwa alipokelewa katika Hospitali ya Mwananyamala na vipimo pamoja na historia yake ilibainisha kuwa ana TB aina ya XDR.
"Ni kweli tumempokea mgonjwa huyo ambaye ni Mtanzania aliyekuwa akitokea Afrika Kusini, na sasa tayari tumempeleka Kibong'oto wilayani Hai mkoani Kilimanjaro kwa matibabu," alisema.
Wakati huohuo, takwimu za Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii zinaonyesha kuwa kuna ongezeko kubwa la wagonjwa wa kifua kikuu ambapo idadi ya watu waliopimwa mwaka 2013 imeongezeka kutoka 11, 640 mwaka 2009 hadi 20,469,241 mwaka 2013.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Dk Grace Maghembe alisema kwa kawaida mgonjwa wa aina hiyo anapopokelewa hupelekwa Kibong'oto kwa matibabu zaidi.
Dk Maghembe alisema kwa sasa wagonjwa wengi wanapelekwa karantini ya Kibong'oto wakati matengenezo ya karantini ya Sinza yakiendelea.
"Tutakapokamilisha karantini hii ya Sinza tutakuwa na uwezo wa kuwahifadhi baadhi ya wagonjwa wa TB sugu hapa jijini," alisema.Kwa sasa wagonjwa wengi walio katika karantini ya Kibong'oto Wilaya ya Hai, Mkoa wa Kilimanjaro, wanaugua Kifua Kikuu sugu aina ya MDR-TB.
Dk Lupinda alisema Afrika Kusini ni miongoni mwa nchi za Afrika ambazo tayari zina wagonjwa wenye kifua kikuu hiki cha XDR.
WHO linaeleza kuwa XDR-TB ni hatari zaidi, kwani mtu anapokuwa nayo haiwezi kutibika hata kwa dawa nyingine za mstari wa pili za kutibu usugu wa maradhi hayo.
Wakati huohuo, WHO limetahadharisha kwamba, ifikapo mwaka 2015 huenda watu milioni mbili duniani wakaambukizwa aina ya kifua kikuu ijulikanayo kama MDR isiyotibika kwa dawa zilizoko sokoni.
Wataalamu wa afya wanasema kwamba, watu wenye ugonjwa wa kifua kikuu aina ya XDR ulio hai mwilini, ikimaanisha kuwa vijidudu mwilini mwao vina uwezo wa kuingia kwa watu wengine ni hatari zaidi hasa katika nchi zenye msongamano wa watu.
TB hai inaweza kusababisha maambukizi kwa watu 10 hadi 15 kwa watu katika kipindi cha mwaka mzima endapo haitatibiwa.
Hapa nchini utafiti wa TB uliofanyika mwishoni mwa mwaka jana, ulibaini kuwa watu wenye umri wa kuanzia miaka 45 na kuendelea wanaathiriwa zaidi.
Wataalamu na madaktari wamefahamu kuwa dawa ambazo zilikuwa huko nyuma zikitumika kutibu TB hivi sasa hazina athari nzuri kwa vijidudu vya ugonjwa huo.
Kumekuwa na wasiwasi mkubwa kuhusu kuenea kwa aina hii ya kifua kikuu ambayo ni sugu na isiyo na dawa.
Aina hiyo imekuwa kakamavu kwa kiasi kikubwa kwa dawa za TB zinazotumika kama chaguo la kwanza (first choice drug) na hata zile za chaguo la pili katika kutibu ugonjwa huo.
TB sugu hutokea pale ambapo bakteria wanaosababisha ugonjwa huo kushindwa kutibiwa na dawa za awali za kawaida.
Endapo TB itashindwa kutibika na dawa za awali, huitwa MDR-TB au Multi-drug resistants. Endapo TB itakuwa sugu baada ya dawa za aina ya pili za kutibu MDR, basi aina hiyo ya TB huitwa 'xtremse drusg resisstant tubersculosis'.Chanzo cha usugu wa TB
WHO inaeleza kuwa XDR-TB ni kifua kikuu hatari zaidi, kwani hakisikii dawa aina yoyote na aghalabu tiba yoyote atakayopewa mgonjwa humletea madhara (side effect).
Pia, WHO inaeleza kuwa mara nyingi XDR-TB hupatikana katika maeneo duniani ambayo TB ya aina hiyo ni maarufu.
Kuhusu namna aina hiyo ya TB inavyopatikana, Dk Lupinda anaonya kuwa maradhi hayo huwapata wagonjwa wa TB wasiofuata kanuni za umezaji wa dawa.
"Pia, wale wasiomaliza dozi, wanaopata TB kwa mara ya pili baada ya kuwa walishatumia dozi, au mtu aliyeishi na mgonjwa mwenye MDR au XDR-TB," anasema.
Usugu wa TB, Dk Lupinda anaelezea kuwa unasababishwa zaidi na wagonjwa kutofuata kanuni za utumiaji wa dawa hali inayosababisha bakteria hao kujizalisha na kuwa na nguvu zaidi ya kutohimili dawa.
Habari mbaya ni kuwa TB sugu huweza kuambukizwa kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine.
Dalili za XDR-TB
Daktari wa magonjwa ya Binadamu wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dk Mhina Elikoheza alisema dalili za TB aina hii ni sawa na zile za TB ya kawaida ambapo mgonjwa hukohoa kikohozi kikavu kwa muda wa wiki moja.
Kadhalika dalili nyingine ni kukohoa makohozi yaliyochanganyika na damu, kutokwa jasho wakati wa usiku na homa za vipindi.
Kuhusu sababu hatarishi, Dk Elikoheza alisema, sababu nyingine inayochangia usugu wa TB ni kufanya kazi katika machimbo bila kuzingatia upimaji na matumizi sahihi ya dawa za kifua.

Wednesday, December 10, 2014

Askofu Desmond Tutu ana tezi dume

Askofu mstaafu Desmond Tutu
Askofu mkuu mstaafu wa Cape Town,Desmond Tutu,ameahirisha mipango ya ziara zake kwa mwaka mzima ujao kutokana na sababu za kiafya.
Taarifa iliyotolewa na taasisi yake imeeleza kuwa Askofu huyo ataanza matibabu hivi karibuni ili kukabiliana na tezi dume ambayo amedumu nayo miaka kumi na mitano iliyopita.
Binti wa Askofu huyo amemuelezea baba yake mwenye umri wa miaka themanini na miwili,kwamba hatahudhuria tuzo za Nobel zitakazo fa

Monday, November 17, 2014

Mafua ya ndege yathibitishwa Uingereza

Ndege wanaofugwa wanakabiliwa na milipuko ya mafua ya ndege
Mlipuko wa mafua ya ndege umethibitishwa katika shamba moja la kuzalishia bata mashariki mwa Yorkshire, nchini Uingereza, wamesema maafisa.
Wizara ya Mazingira, Chakula na Masuala ya Vijijini (Defra) imesema hatari kwa afya ya umma ni ndogo sana. Ndege wasiohitajika wanaondolewa kutoka eneo hilo na eneo la kuwatenga limeandaliwa.
Tatizo hilo bado halijathibitishwa, lakini aina ya kirusi cha H5N1 hakijaweza kubainishwa na maafisa wa Defra.
Kirusi hicho husambaa kati ya ndege na katika matukio ya nadra, kinaweza kuwaathiri binadamu.
Picha ikimwonyesha mchuzi akiuza bata wake katika mtaa mmoja mjini Shanghai,China
Eneo la kuwatenga ndege lililopo kuzunguka shamba hilo litazuia ndege na kinyesi cha ndege ndani au nje ya eneo hilo.Ndege wote pia watatengwa.
Mlipuko wa ugonjwa hatari wa mafua ya ndege uligundulika Jumapili katika shamba moja nchini Uholanzi.
Tukio hili huko Yorkshire ni la kwanza nchini Uingereza tangu mwaka 2008, wakati ulipozuka. Mafua ya ndege daima yamekuwa yakidhibitiwa kikamilifu nchini Uingereza.
Msemaji wa wizara amesema: "tumethibitisha tukio la mafua ya ndege katika shamba la kuzalishia bata huko Yorkshire - afya za watu haziko katika hatari na hakuna hatari katika vyakula. "Tunachukua hatua za dharura katika kukabiliana na janga hili ambazo zinahusisha eneo la kilomita 10 na kuwaondoa ndege wote katika shamba kuzuia uwezekano wa kusambaa kwa mambukizi. Uchunguzi wa kina kuhusu ugonjwa huo unaendelea.
Tuna rekodi nzuri ya udhibiti na utokomezaji wa milipuko ya ugonjwa wa ndege iliyowahi kutokea siku za nyuma nchini Uingereza

Wednesday, October 1, 2014

Waliodhurika kwa togwa Songea sasa wafikia watu 340




Idadi ya watu waliolazwa hospitalini kwa kunywa togwa inayosadikiwa kuwa na sumu katika 
Kijiji cha Litapwasi, Kata ya Mpitimbi mkoani Ruvuma imeongezeka kutoka 270 hadi 340.
Tukio hilo lilitokea Jumapili baada ya watu kushiriki sherehe ya Kipaimara ambako walikula, 
kunywa pombe na togwa na baadaye wale waliokunywa togwa walianza kuumwa matumbo, 
kuhara na kutapika.
Hadi jana, watu 102 walikuwa bado wamelazwa katika Zahanati ya Lyangweni, Hospitali ya 
St. Joseph Peramiho na Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma.
Tayari watu watano wanashikiliwa na Polisi kwa upelelezi kuhusiana na tukio hilo, 

akiwamo Baba Mzazi wa mtoto Dickson aliyepata kipaimara, Enes Nungu (47).(T.K)
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Mihayo Mskhiela aliwataja watu wengine 
wanaoshikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Songea kwa mahojiano kuwa ni 
Benedict Nungu (76), Esebius Komba (36), Sadiki Masodi (65) na John 
Kaulangudidi. Mtu anayedaiwa kukabidhiwa ufunguo chumba cha vinywaji kabla 
ya kugawiwa kwa wananchi, Ridhiwani Shawa haijulikani alipo.
Mabaki ya chakula, togwa na pombe ya kienyeji vilichukuliwa juzi na kupelekwa 
kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kwa uchunguzi.
Kamanda Mskhiela alitoa wito kwa wananchi wanaoandaa sherehe kuhakikisha 
wanafanya hivyo katika mazingira mazuri na yenye usalama ili kuepuka athari kama hizo.
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Peramiho, Dk Vanace Mushi alisema hadi 
jana, watu waliokuwa wamelazwa katika hospitali hiyo walikuwa 34 na hakukuwa 
na mgonjwa aliyeruhusiwa kurudi nyumbani.
Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma, Majuto Mlawa 
alisema wagonjwa tisa wa rufaa walipokewa na kupatiwa matibabu huku hali zao 
zikiwa mbaya.
Akizungumzia tukio hilo, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu alisema:
 "Jambo hili limenisikitisha sana, nimeumizwa sana nawapa pole wote 
waliopatwa na tatizo hilo naamini Mwenyezi Mungu atawasaidia na watapona 
na kurejea katika hali zao za kawaida."
Hata hivyo, Mwambungu alisema hiyo ni ajali kama nyingine, hivyo anaviachia 
vyombo vya usalama na wataalamu wa afya kupata ukweli. Pia aliwataka 
wananchi kuwa makini pindi wanapoandaa vyakula na pombe za kienyeji katika 
sherehe mbalimbali.
TUPAMBANE BLOG