Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Tuesday, September 2, 2014

Oh! Oh! Mtoto Niliyemwona Harare 1989 Leo Amefunga Ndoa..!


  • Written by Tupambane Blog
  • Email
  • Tuma Maoni
  • Share on facebook Share on google_plusone_share Share on twitter
Ndugu zangu,
Ni Ipelanya Kulwa, wa kwanza kushoto kwenye picha ya pili. Pichani ni Harare, Zimbabwe, Desemba, 1989. Ipelanya alikuwa mdogo sana wakati huo, labda miaka 9 au 10. Mapema mwaka huu niliiweka picha hii kwenye fb, naye akajitambua. Akanipigia simu. Alishangaa sana kuiona picha yake. Hakuwa hata na kumbukumbu kuwa nilipata kutembea nae mitaa ya Harare akiwa na mtoto mwenzake.
Na mimi niliiweka picha hiyo bila kuwa na kumbukumbu ya majina ya watoto hao. Na bado ningependa kujua huyomtoto wa pili ni nani. Ipelanya ametaka kujua zaidi ya wakati huo. Nakumbuka Baba yake alikuwa Mtaalamu wa mawasilino ya simu. Wakati huo, Zimbabwe iliomba wataalamu wa maeneo mbali mbali kutoka Tanzania.
Na hakika, Zimbabwe ilikuwa nchi changa sana.Ilikuwa na miaka 6 tu ya Uhuru. Na mimi nilikuwa ndio kwanza nimemaliza Form Four pale Tambaza Sekondari. Tangu enzi nikiwa shuleni , nilipenda sana kufuatilia masuala ya harakati za Ukombozi Kusini mwa Afrika. Nilifika Lusaka pia, Zambia. Nikiwa Zimbabwe sikuishia Harare tu, nilifika maeneo ya vijijini pia. Nilifika Nyanga, Mberengwa, jirani na mpaka wa Msumbiji, na hata Bulawayo.
Nikiwa Nyanga niliona nini maana ya jamii zilizokuwa zikiishi katika mifumo ya kibaguzi. Mji unakuwa na sehemu mbili; ya Wazungu na Weupe. Kwenye Township ndiko walikoishi Makabwela.
Kwenye Maktaba yangu bado nina picha kadhaa za wakati huo. Moja nimepiga nje ya nyumba ya Ipelanya Harare, nikiwa na dada yake Ipelanya. Ipelanya ameniambia dada yao amebaki Zimbabwe na ameolewa huko, miaka yenda mbio kweli!
Hongera Ipelanya kwa kufunga ndoa! Na kule Zimbabwe wanasema Makorokoto!
Maggid

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG