Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Sunday, October 19, 2014

Simba dakika 35 za hatari sana

  • Written by Tupambane Blog
  • Share on facebook Share on gmail Share on twitter 
Wachezaji wa Simba wakijadiliana jambo uwanjani
KIKOSI cha Simba kina silaha moja hatari ambayo kama Yanga watashindwa kugundua, wataumia ndani ya dakika 35 za mwanzo, lakini dakika za mwisho za kipindi cha pili Simba huchoka.
Katika mechi tatu za Ligi Kuu Bara ambazo Simba imecheza chini ya Kocha, Mzambia Patrick Phiri wamefanikiwa kupata mabao ya mapema kati ya dakika ya kwanza mpaka 35 za mchezo.
Lakini pamoja na ubora wao huo dakika za mwanzoni, imekuwa na tatizo la kuzidiwa na timu pinzani katika dakika za mwishoni ambazo ndiyo ziliwalazimisha wakatoa sare katika mechi zao tatu za ligi.
Katika mechi hizo, walipofungua ligi dhidi ya Coastal wakatoa sare ya 2-2, Simba ndiyo ilianza kufunga mabao yote mawili ambayo yalifungwa na Shaaban Kisiga dakika ya saba na Mrundi Amissi Tambwe aliyefunga la pili dakika ya 32.
Lakini kipindi cha pili Coastal walisawazisha mabao yao kupitia kwa Yayo Lutimba raia wa Uganda dakika 66 na Mkenya Ramadhani Salim 'Rama' alifunga la pili dakika 81.
Mechi ya pili dhidi ya Polisi Morogoro, Simba ndiyo ilianza kufunga bao lake dakika ya 32 kupitia kwa Emmanuel Okwi raia wa Uganda lakini maafande hao, walisawazisha bao hilo kipindi cha pili dakika ya 50 kupitia kwa Danny Mrwanda matokeo yakawa 1-1.
Stendi nayo iliwaotea Simba kwa staili hiyo hiyo wakatoa sare ya 1-1. Wekundu hao wa Msimbazi walifunga bao lao dakika ya 35 kupitia kwa Shaaban Kisiga na Stendi ilisawazisha dakika ya 45 kupitia kwa Kheri Mohamed.
Phiri aliwahi kukiri kuwa kikosi chake hicho kina tatizo la kucheza vizuri kipindi cha kwanza lakini kipindi cha pili huwa hawafanyi vizuri, jambo ambalo aliahidi kulitafutia ufumbuzi.
Ushindi wa mechi tatu za Yanga walioupata kwa Tanzania Prisons matokeo yakawa 2-1, mabao yao yalifungwa dakika ya 18 na Andrey Coutinho na Simon Msuva alifunga la pili dakika ya 70.
Matokeo ya 2-1 walipoifunga JKT Ruvu, mabao yao yalifungwa dakika ya 35 na Kelvin Yondani na Mnyarwanda Haruna Niyonzima alimalizia la pili dakika ya 68

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG