Mwanamuziki Amour Genius.
QS Mhonda J Entertainment imempeleka msanii wake chipukizi aitwaye AMOUR GENIUS nchini Afrika Kusini kufanya video ya wimbo wake mpya uitwao WANIMALIZA ambao amemshirikisha ‘hit maker’ wa wimbo wa MAUMIVU – KADJA NITO.
Meneja wa kampuni hiyo, Fredy Felix, amethibitisha hayo ambapo alisema mashabiki wakae mkao wa kupokea video nzuri kutoka kwa AMOUR.
Pia Fredy aliongeza kuwa yote hayo ni matayarisho ya QS INTERNATIONAL MUSIC BAND ambayo inaundwa na Q-CHILLAH, MB DOG, KADJA NITO, SHALVINY na AMOUR.
Bendi hiyo inatarajiwa kuzinduliwa mapema mwakani ambapo kwa sasa wasanii wake wapo wanajinoa ili kutoa vibao vikali ambavyo vitakonga nyoyo za mashabik
No comments:
Post a Comment