Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Sunday, December 7, 2014

KITUO CHA RADIO 5 WAANDA “KAMPENI YA RADIO 5 VIWANJANI”MSIMU HUU WA SIKUKUU YA XMASS NA MWAKA MPYA


SAM_0369
Radio 5 FM 105.7 imeandaa “kampeni ya RADIO 5 viwanjani” katika mkoa wa Arusha ambapo itawakutanisha watangazaji  na madjs na wasikilizaji wao katika kumbi za starehe kwa takribani wiki tano ikiwa ni sehemu ya kuwashukuru mashabiki wa Redio hiyo kwa kuwa pamoja kwa mwaka mzima huku mashabiki wakijipatia zawadi mbalimbali katika kampeni hiyo(katika picha ni Mtangazaji wa kituo cha Redio 5 Julius Kamafa aliyejizolea umaarufu mkubwa jijini Arusha kupitia kipindi chake cha funiko base kinachosikilizwa zaidi na vijana akishow love na msikilizaji wake katika kampeni  ya “Redio 5 viwanjani”ndani ya ACTIVE CLUB – Mbauda jijini Arusha
SAM_0349
Timu kazi ya Redio 5 wakifatilia show 
SAM_0350
Mtangazaji maarufu aliyejizolea umaarufu mkubwa  kupitia kipindi chake cha love cuts Semio Sonyo akiwa anauliza maswali kwa vijana wa Arusha waliofika katika kampeni ya Redio 5 viwanjani ndani ya ACTIVE CLUB – Mbauda jijini Arusha
SAM_0358
Meneja  ubunifu wa Redio 5 Vicky Mwakoyo akifurahia jambo katika kampeni ya Redio 5 viwanjani iliyofanyika jijini Arusha
SAM_0353
Mtangazaji maarufu aliyejizolea umaarufu mkubwa  kupitia kipindi chake cha love cuts Semio Sonyo akimuuliza maswali shabiki wa redio 5 katika kampeni ya Redio 5 viwanjani yenye nia ya kuwashukuru wasikilizaji wa kituo hicho kwa kuwa pamoja kwa mwaka mzima
SAM_0383
Meneja  ubunifu wa Redio 5 Vicky Mwakoyo kushoto akieleza nia ya kampeni hiyo itakayofanyika katika bar mbalimbali jijini hapa ambapo pia wasikilizaji wa kituo hicho watajizolea zawadi mbalimbali zikiwemo T-shart,vikombe,vinywaji kutoka TBL

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG