Radio 5 FM 105.7 imeandaa “kampeni ya RADIO 5 viwanjani” katika mkoa wa Arusha ambapo itawakutanisha watangazaji na madjs na wasikilizaji wao katika kumbi za starehe kwa takribani wiki tano ikiwa ni sehemu ya kuwashukuru mashabiki wa Redio hiyo kwa kuwa pamoja kwa mwaka mzima huku mashabiki wakijipatia zawadi mbalimbali katika kampeni hiyo(katika picha ni Mtangazaji wa kituo cha Redio 5 Julius Kamafa aliyejizolea umaarufu mkubwa jijini Arusha kupitia kipindi chake cha funiko base kinachosikilizwa zaidi na vijana akishow love na msikilizaji wake katika kampeni ya “Redio 5 viwanjani”ndani ya ACTIVE CLUB – Mbauda jijini Arusha
Timu kazi ya Redio 5 wakifatilia show
Mtangazaji maarufu aliyejizolea umaarufu mkubwa kupitia kipindi chake cha love cuts Semio Sonyo akiwa anauliza maswali kwa vijana wa Arusha waliofika katika kampeni ya Redio 5 viwanjani ndani ya ACTIVE CLUB – Mbauda jijini Arusha
Meneja ubunifu wa Redio 5 Vicky Mwakoyo akifurahia jambo katika kampeni ya Redio 5 viwanjani iliyofanyika jijini Arusha
Mtangazaji maarufu aliyejizolea umaarufu mkubwa kupitia kipindi chake cha love cuts Semio Sonyo akimuuliza maswali shabiki wa redio 5 katika kampeni ya Redio 5 viwanjani yenye nia ya kuwashukuru wasikilizaji wa kituo hicho kwa kuwa pamoja kwa mwaka mzima
Meneja ubunifu wa Redio 5 Vicky Mwakoyo kushoto akieleza nia ya kampeni hiyo itakayofanyika katika bar mbalimbali jijini hapa ambapo pia wasikilizaji wa kituo hicho watajizolea zawadi mbalimbali zikiwemo T-shart,vikombe,vinywaji kutoka TBL
No comments:
Post a Comment