- Written by Tupambane Blog
-
Share on facebook Share on gmail Share on twitter

Jana kupitia media nilipata nafasi kidogo ya kufuatilia kwa karibu sakata la Miss Tanzania Sitti Mtemvu na tuhuma za kudanganya umri.
Imenikumbusha kisa cha mchezaji wa Simba Noordin Bakari aliyecheza mechi za Caf ikiwamo mechi na Zamalek kwa kusajiliwa akiwa na miaka 23. Ajabu kwenye michuano mingine ya Caf chini ya miaka 21, Noordin huyo huyo akaibuka kwenye Serengeti Boys akitajwa kuwa ana miaka 17! Na ajabu ya media yetu, baadhi ya wanahabari wakatetea uongo ule.
Nakumbuka nilipoandika makala kushutumu uongo ule wa kuaibisha taifa, kuna walionipigia simu na kuniambia nimekosa uzalendo!
Maggid
No comments:
Post a Comment