Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA
Showing posts with label ccm. Show all posts
Showing posts with label ccm. Show all posts

Thursday, July 28, 2016

MWENYEKITI WA CCM RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA SEKRETARIETI NA WAFANYAKAZI WA CHAMA DODOMA MJINI DODOMA


1Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akilakiwa mara baada ya kuwasili makao makuu ya chama hicho mjini Dodoma leo
2Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akijiandaa kuongea na sekretarieti ya CCM kwa mara ya kwanza katika  makuu ya chama hicho mjini Dodoma leo.
3 4Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiongea na wafanyakazi wa  makao makuu ya chama hicho mjini Dodoma leo.
7Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiwa na Katibu Mkuu wa CCM Ndg Abdulrahman Kinana akisikiliza maoni na changamoto toka kwa wafanyakazi wa  makao makuu ya chama hicho mjini Dodoma leo.
5Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Waziri Mkuu Ndg. Kassim Majaliwa katika picha ya pamoja na Secretarieti ya CCM  makao makuu ya chama hicho mjini Dodoma leo.
6Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Waziri Mkuu Ndg. Kassim Majaliwa katika picha ya pamoja na Sekretarieti ya CCm na wafanyakazi wa makao makuu ya chama hicho mjini Dodoma leo.
8Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiaga baada ya kupata picha ya pamoja na Sekretarieti ya CCm na wafanyakazi wa makao makuu ya chama hicho mjini Dodoma leo.

Monday, September 29, 2014

‘Katiba itaibeba CCM Zanzibar’



Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ),
Mohamed Aboud Mohamed amesema Katiba inayopendekezwa, itaibeba CCM katika 
uchaguzi mkuu ujao visiwani humo.
Akizungumza katika mahojiano maalumu bungeni jana, Aboud alisema katiba hiyo 
 itawasaidia katika kujibu kero mbalimbali zilizokuwa zikitolewa kwani imejibu 
asilimia 90 ya kero hizo.
"Kwa asilimia zaidi ya 90 kero za muda mrefu za wananchi wa Zanzibar zimejibiwa. 
Kwa hiyo wananchi watajua kuwa tumeshughulika na kero zao kwa kuzipatia 
ufumbuzi,"alisema.
Aboud alisema watakwenda kwa wananchi wa Zanzibar wakiwa kifua mbele 
kufafanulia kero ambazo zimetafutiwa ufumbuzi na wajumbe wa Bunge la 
Katiba, wengi wao wakitokana na CCM.
"Mimi ninaamini kuwa wananchi wakipelekewa Rasimu ya Katiba hii 
 inayopendekezwa na wakaiona kuwa imekidhi matakwa yao wataiunga 
mkono,"alisema Aboud katika mahojiano hayo.
Aeleza kuhusu urais 2015 (t.k)
Waziri huyo ambaye aliwahi kuwania nafasi ya urais wa Zanzibar mara mbili 
 (mwaka 2000 baada ya Dk Salmin Amour kumaliza muda wake na mwaka 2010 
 wakati Amani Abeid Karume alipokuwa akiondoka madarakani), alisema 
 hatagombea tena nafasi hiyo katika uchaguzi mkuu ujao wa 2015.
"Sina nia wala dhamira ya kugombea tena urais. Mimi dhamira yangu kubwa 
ilikuwa ni kuiunganisha Zanzibar kazi ambayo Rais aliopo (Dk Ali Mohamed Shein) 
ameifanya vizuri,"alisema.
Aboud alisema sifa ya Rais ni uadilifu na kuwaunganisha Wazanzibari na 
Watanzania kwa jumla, sifa ambazo zote amekuwa nazo Rais wa Serikali ya 
 Mapinduzi ya Zanzibar Dk Shein. Hata hivyo, alisema kazi yoyote 
inayofanywa na mwanadamu inakuwa na upungufu, haiwezi kuwa kamili.
"Mimi nina uhakika matarajio ya Wazanzibari yamepata majibu katika 
Rasimu hii ya Katiba. Na ninaamini kuwa wataipokea vizuri. Lazima 
tufahamu kuwa Katiba ni mchakato," alisema.
Aboud alisema kama kuna jambo ambalo hawakulipata katika mchakato 
wa sasa wa Katiba unaomalizika Oktoba 4 au hawakufikia mwafaka , 
kesho wanaweza kupata nafasi ya kulizungumza.
Alipoulizwa kero zilizopatiwa ufumbuzi katika Katiba hiyo, Aboud aliitaja 
kero ya mafuta na gesi ambapo sasa Zanzibar itakuwa na uwezo wa kushughulikia.
"Zanzibar sasa itaweza kutunga sheria na sera zake za kushughulikia mafuta 
na gesi, lingine lilikuwa ni ushiriki wa Zanzibar katika taasisi za 
kimataifa," alisema Aboud.
Alisema Rasimu imetoa haki ya Zanzibar katika mikopo na imetoa fursa ya 
kupunguzwa kwa mambo ya muungano ambayo ilikuwa ni sehemu ya kero 
ya Wazanzibari.
Ukawa kuondoka bungeni
Aboud alisema Ukawa na wajumbe wanaotokana na CUF, kususia Bunge hilo, 
hiyo haitaathiri uendeshaji wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa kwa vile bado 
wana umoja.
"Hawa walijitoa si kwa sababu hawaoni umuhimu wa Bunge la Katiba. 
Walijitoa kwa sababu waliamini suala la serikali tatu ni suala la msingi. 
Sisi tumeona mfumo wa Serikali mbili ndiyo utakaodumisha muungano," 
alisema na kuongeza:
"Sisi tumejali sana masilahi ya wananchi, sasa wao pengine wamejali sana 
masilahi yao. Sisi tumeona kuwa mfumo wa serikali mbili ndiyo utaweka 
msingi wa muungano."
Alisema pengine CUF wamejali sana faida watakazopata kutokana na mfumo 
wa serikali tatu.
"Wanajua wao kwa nini wanataka mfumo wa Serikali tatu. Lakini kwa mimi na
 imani kabisa serikali mbili ndiyo njia sahihi," alisema Aboud.

Tuesday, September 9, 2014

NAPE ATOA DARASA KWA VIONGOZI WA CCM UINGEREZA


  • Written by  Tupambane Blog
  • Email
  • Tuma Maoni
  • Share on facebook Share on google_plusone_share Share on twitter 

Katibu wa NEC itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye akizungumza na viongozi wa mashina ya CCM Uingereza  ambapo aliwaambia matawi ya CCM nje ya nchi yawe mawakala wa kuleta mabadiliko ndani ya chama pamoja na kuwaunganisha watanzania kujikomboa kiuchumi
Baadhi ya viongozi wa mashina ya CCM Uingereza wakifuatilia mafunzo kutoka kwa Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye aliyekuwa akitoa somo juu ya Wajibu wa Matawi ya CCM nje ya Nchi.

 Viongozi wa mashina wakisikiliza kwa makini.(P.T)

 Viongozi wa mashina ya CCM nchini Uingereza wakiandika pointi muhimu.

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi wa mashina ya CCM nchini Uingereza .

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi wa mashina ya CCM London nchini Uingereza mara baada ya kutoa somo linalohusu Wajibu wa Matawi ya nje ya CCM katika ukumbi wa kituo cha mafunzo Barking,London ya mashariki.

Katibu wa NEC Itikadi na Unezi Nape Nnauye akijibu  maswali mbalimbali kutoka kwa mwandishi maarufu nchini Uingereza Ayoub Mzee mara baada ya kumaliza kutoa semina kwa viongozi wa mashina ya CCM nchini Uingereza
TUPAMBANE BLOG