Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Sunday, January 4, 2015

Msichana anusurika ajali ya ndege




Ajali ya ndege
Mtoto mmoja wa miaka saba ametembea hadi katika nyumba moja katika jimbo la Kentucky nchini Marekani ili kuripoti kuanguka kwa ndege aliyoabiri.
Kulingana na polisi ndege hiyo baadaye ilipatikana imeanguka huku watu wanne wakiwa wamefariki katika kaunti ya Lyon yapata kilomita 50 mashariki mwa mji wa Paducah
Kituo cha runinga cha NBC nchini Marekani kimesema kuwa msichana huyo alimwarifu mtu aliyemfungulia mlango kwamba wazazi wake walifariki katika ajali hiyo ya ndege.
Picha ya ndege hiyo haijatolewa na polisi hawajatoa tamko lolote kuhusu uhusiano wake na waathirwa.
Shirika linalosimamia anga za juu limesema kuwa maafisa wanaodhibiti usafiri wa ndege walipoteza mawasiliano na ndege hiyo aina ya Piper PA-34 baada ya rubani kuripoti matatizo ya mitambo.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG